Mpaka 2015 kulikua na Watu Milioni moja laki 4 wanaoishi na VVU Tanzania. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Thursday, December 29, 2016

demo-image

Mpaka 2015 kulikua na Watu Milioni moja laki 4 wanaoishi na VVU Tanzania.

.com/simgad/
tacaids
December 28,2016 Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania-TACAIDS kupitia kwa Mkurugenzi Mtendaji wake, Dkt Leonard Maboko amezitoa takwimu za hali ya VVU na UKIMWI Tanzania kulingana na hali Duniani na ya ukanda wa mashariki na kusini mwa Afrika.
 Taarifa aliyoitoa Dkt Maboko imeeleza kuwa……''

1.Watu waishio na VVU kwa mwaka 2015 Tanzania walikuwa takribani milioni 1.4.

2.Watu wanaotumia dawa za kupunguza makali ya VVU hadi kufikia June 2016 Tanzania walikuwa takribani 800,000.

3.Inakadiriwa mwaka 2015 nchini Tanzania kati ya watu 54,000 waliambukizwa virusi vya UKIMWI.

4.Kiwango cha maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI kimeshuka kwa zaidi ya 20% kati ya mwaka 2010- 2015.

Dkt. Maboko alisema, Ukimwi bado ni janga kubwa duniani na taifa kwa ujumla huku akitaja kundi la wanawake kuwa ndilo lina kiwango cha juu cha maambukizi ya VVU huku mikoa ya Njombe, Iringa na Mbeya ukiwa na kiwango cha juu cha maambukizi hayo Kitaifa.


Aidha, alisema serikali imejiwekea mikakati kuhakikisha kuwa waliogundulika kuwa wameathirika wanaanzishiwa dawa, kuhimiza matumizi ya mpira wa kiume, kupunguza maambukizi mapya kwa asilimia 29 na kutoa elimu kwa wanawake wanaojihusisha na ngono, kupunguza maambukizi ya virusi vya Ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.
   

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *