|
Nao Manchester
United waliitandika Bournemouth Bao 3-1 na kuamsha shangwe za Mashabiki wao
kuimba 'Jose Mourinho' mwishoni mwa Mechi.
Man United
walifunga Bao lao la kwanza Dakika ya 40 baada ya pasi ndefu ya Ander Herrera
kuwahiwa na Beki wa Bournemouth Simon Francis ambae alitoa nyuma kumrudishia
Kipa wake Boruc lakini Juan Mata akainasa na Kipa Boruc kuokoa na Mpira
kumgonga Simon Francis na kurudi tena kwa Mata aliefunga kilaini.
Dakika ya 59
Kepteni Wayne Rooney akapiga Bao la Pili kwa Kichwa baada ya Krosi ya Valencia
kuunganishwa fyongo na Anthony Martial na kumkuta Rooney aliemalizia hadi
wavuni.
Bao la 3 la
Man United lilipachikwa na Mchezaji Mpya Zlatan Ibrahimovic katika Dakika ya 64
na kuwa Bao lake la kwanza kwa Klabu yake mpya.
Adam Smith
aliipa Bournemouth Bao lao pekee Dakika ya 64 na Mechi kwisha kwa Bournemouth kufungwa bao 1-3 na Man
United .
|
No comments:
Post a Comment