MATOKEO / RATIBA VPL 2015/2016:-Mwadui FC yaikabidhi rasmi Yanga SC kombe la VPL baada ya kuichapa Simba SC kwa bao 1-0. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, May 08, 2016

MATOKEO / RATIBA VPL 2015/2016:-Mwadui FC yaikabidhi rasmi Yanga SC kombe la VPL baada ya kuichapa Simba SC kwa bao 1-0.

Simba SC imefungwa Bao 1-0 na Mwadui FC huko Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam na kuupeleka Ubingwa wa Msimu huu kwa Yanga ambao Leo,May 08,2016 hawakucheza na ambao wana Mechi 3 mkononi.

Bao ambalo liliiua Simba SC lilifungwa Dakika ya 73 na Jamal Nyate katika Mechi ambayo kwenye Dakika za Majeruhi Mchezaji wa Simba Ajib alitolewa kwa Kadi Nyekundu kwa Rafu mbaya.

 Simba SC ndio ilikuwa Timu pekee ambayo ingeweza kuikamata Yanga SC lakini kipigo chao cha Leo kimewaacha na Pointi 58 na hata wakishinda Mechi zao zote 3 zilizobaki hawawezi kuwafikia Yanga wenye Pointi 68.

Nako huko Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, Azam FC walitoka nyuma 1-0 kwa Bao la Dakika ya 24 la Adam Kingwande na kuichapa Kagera Sugar kwa Bao za Kipindi cha Pili za Kipre Tchetche na Himid Mao za Dakika za 46 na 59 ambazo ziliwapa ushindi wa 2-1.

Azam FC sasa wamekamata Nafasi ya Pili wakiwa na Pointi 60 na wamebakisha Mechi 2.

LIGI KUU VODACOM

Msimamo – Timu za Juu:

1 Yanga Mechi 27 Pointi 68

2 Azam FC Mechi 28 Pointi 60

3 Simba Mechi 27 Pointi 58

LIGI KUU VODACOM

RATIBA:                                               

Jumanne Mei 10

Mbeya City v Yanga

Jumatano Me 11

Majimaji v Simba

Jumamosi Mei 14

Mgambo JKT v JKT Ruvu

Ndanda FC v Yanga

Jumapili Mei 15

Mtibwa Sugar v Simba

Kagera Sugar v Stand United

Mwadui FC v Mbeya City


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad