Jana, akiongea na viongozi wa ngazi
tofauti wa CCM katika hafla ya kuwashukuru kwa kazi waliyoonyesha wakati wa
Uchaguzi Mkuu uliopita, Rais Magufuli alisema kama watu anaowatumbua hadharani
pia waliiba hadharani, ni lazima watumbuliwe hadharani.
Magufuli alisema kuwa mateso
waliyopata mamilioni ya Watanzania kutokana na kuibiwa, yanafanywa na hao
wachache lazima nao waanze kupata mateso hayohayo.
“Kwa hiyo ziko haki za binadamu kwa
matajiri tu kwa hawa walioibiwa hakuna haki,” aliuliza Rais Magufuli.
“Kwa hiyo unaweza kuona hawa
wanaowatetea nao ni majipu. Tutaanza kuwafuatilia. Hata ukimtoa huyo, nikimsema
hadharani wanasema eti nimefanya kosa.”
Rais Magufuli alisema kwa bahati
nzuri aliwateua yeye na kuwatangaza hadharani, hivyo akahoji sababu za
kutotangazwa hadharani siku ya kutenguliwa kwa kuwa ndiyo saizi yake
aliyewateua.
“Kama ni mkurugenzi wa manispaa au wa
wapi nimemteua mimi. Eti wanasema apewe muda wa kujieleza. Ajieleze yeye
aliwapa muda wananchi kujieleza alipokuwa anawaibia? Napenda niwahakikishie
tutaendelea kusimama imara,” alisema Dk Magufuli.
Zaidi, msikilize kwenye video Hapo
Juu.
No comments:
Post a Comment