|
Mkuu wa shule hiyo Bw.Aaron Dishon
Sekazoya ( Pichani ) amesema jitihada zilizofanywa na shule hiyo ni kukarabati
madawati 150 na vitanda 46 kwa thamani ya Sh150 000 na kwamba kanisa la
Anglikan wilayani Ngara kupitiaTumaini Fund utajenga matundu 10 ya vyoo kwa
thamani ya Sh40 milioni.
Bw.Sekazoya amesema changamoto
zilizotajwa za kukosa bwalo na ukumbi wa
mikutano ni pamoja na uhaba wa Hostel, kwani iliyopo ni moja yenye kutosheleza
wanafunzi 90 tu na mabweni yapo mawili na kuhitajika mabweni matatu.
Amesema shule hiyo inahitaji vitanda 200
vya wanafunzi vilivyopo 174
vinavyotumiwa na wanafunzi 87 walioko
katika hostel tatu nab ado mahitaji ni
nyingine tatu zenye kutumiwa na wanafunzi 240
Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu
Tanzania Dr Elia Kibwa ambaye ni mkazi wa wilaya ya Ngara ambaye alikuwa mgeni
rasmi katika mahafali hayo ,
amesema walimu waandae mazingira ya
wanafunzi kwa kupanda miti ambayo itawasaidia kupata zana za kufundishia
Aidha amesema akiwa ndiye mwalimu wa
kwanza katika shule hiyo mwaka 1990
ndoto zake ni wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi
sita kujengwa kisaikolojia kuingia
katika Chuo Kikuu kwa kuwa na ujuzi kupitia masomo ya Sayansi.
“Ndoto zangu nahitaji watakaomaliza
kidato cha sita hapa waingie Chuo kikuu katika
wilaya yetu ili wazawa wapate
wageni kutoka wilaya na mikoa mingine na kujifunza mila na tamaduni za makabila
mbalimbali” Alisema Dr Elia Kibwa.
Katika hatua nyingine amesisitiza
walimu kuwafundisha wanafunzi masomo ya Sayansi , Teknolojia ya Habari na
Mawasiliano TEHAMA ili kuingia katika ushindani wa kimawasiliano katika
kujifunza wakitumia mitandao na kompyuta
HABARI/PICHA Na:-Shaaban Ndyamukama-Ngara/Kagera.
|
No comments:
Post a Comment