HAPA KAZI TU:- Serikali ya Rais Magufuli yakusanya zaidi ya trilioni 1 February 2016 na kugawanywa kwenye Miradi ya Maendeleo. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, February 23, 2016

HAPA KAZI TU:- Serikali ya Rais Magufuli yakusanya zaidi ya trilioni 1 February 2016 na kugawanywa kwenye Miradi ya Maendeleo.

Serikali imefanikiwa kukusanya zaidi ya shilingi trilioni moja kwa mwezi huu wa February ,tofauti na zilizokuwa zikukusanya hapo awali za bilioni 850 kwa kipindi cha mwezi mmoja na kuzielekeza fedha hizo kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo.

Takwimu hizo zimetolewa Jana ,February 22,2016, jijini Dar es salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango  Dkt. Servacius Likwelile wakati akitoa taarifa ya hali ya mapato kwa kipindi cha mwezi Februari mwaka huu,2016.

Dkt. Likwelile amesema ‘kati ya fedha hizo ,sekta ya elimu imepewa shilingi bilioni 18.7  kwa ajili ya utekelezaji wa utoaji wa elimu bure kwa wanafunzi wa shule za awali hadi kidato cha Nne ambapo fedha hizo ni kwa ajili ya malipo ya ada,chakula pamoja na ruzuku‘.

 Mkoa wa Dar es salaam  imeongezewa shilingi bilioni 2 ili kupanua uwezo wa udahili kama Rais alivyoahidi katika mkutano wake na Wazee wa Mkoa huo na kati ya fedha hizo  wakufunzi wamepatiwa shilingi milioni 431.6 walimu walio masomoni wametengewa  shilingi milioni 249.2 kwa ajili ya vifaa vya kufundishia, posho na nauli

fedha nyingine kati ya hizo kiasi cha shilingi bilioni 573.7 zimetolewa kwa ajili ya  mishahara ya watumishi wa Umma  , ulipaji wa deni la taifa kwa mwezi huu zimetolewa shilingi bilioni 842.1 na Mifuko ya hifadhi za Jamii zimetolewa shilingi bilioni 81.13‘.....Unaweza kumtazama hapa Katubu Mkuu Dkt. Servacius Likwelile''.


Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na Mimi Hapa...FACEBOOK .. TWITTER .. INSTAGRAM … Pia Usisite kututumia tukio la Picha/Habari  kwa WhatsApp +255789925630  Or  +255756830214. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad