Vurugu zimetokea katika eneo la Mbagala jijini Dar Es Salaam kufuatia mtoto mwenye umri wa miaka 14 kudaiwa kukidhalilisha kitabu kitukufu cha dini ya kiisilaam Qur’uan huku mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Bw Said Meck Sadick amewataka wakazi wa jiji la Dar es salaam kuwa na subira kwa wakati huu. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, October 12, 2012

Vurugu zimetokea katika eneo la Mbagala jijini Dar Es Salaam kufuatia mtoto mwenye umri wa miaka 14 kudaiwa kukidhalilisha kitabu kitukufu cha dini ya kiisilaam Qur’uan huku mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Bw Said Meck Sadick amewataka wakazi wa jiji la Dar es salaam kuwa na subira kwa wakati huu.


Ndugu Hamis Salum baba wa mtoto ambaye Quran yake imekojolewa.



Mji wa  MBAGALA na vitongoji vyake Jijini Dar es Salaam umekumbwa na  fujo, vurugu na visasi baada ya mtoto wa kiume anayedaiwa kusoma kidato cha pili kukojolea kitabu kitakatifu cha QURUAN.

Vurugu hizo zimetokea  eneo la Mbagala Kizuiani ambapo baadhi ya Waislamu wameandamana kupinga kitendo cha kijana huyo na kupelekea jeshi la polisi kupiga mabomu ya machozi kuwatawanya waandamanaji hao.


Waumini hao ambao wamejiunga kutoka maeneno mbalimbali ya Mbagala wamezingira kituo cha Polisi cha Kizuiani ambapo mtoto amesalimishwa kutokana na sababu za kiusalama.




Waumini hao wenye hasira wanataka kijana huyo atolewa kituoni hapo la sivyo watachoma moto kituo hicho.


Aidha kumeshuhudia vurugu kubwa kutoka Mbagala Kizuiani majira ya saa 7 na sasa inadaiwa wakazi waishio maeneno ya Mbagala wametandwa na hofu kutokana na vurugu hizo.



Mkazi mmoja kutoka maeneo ya Mbande amesema  kuwa tayari kuna baadhi ya watu wameshajeruhiwa na fujo hizo zilitokea maeneo hayo kufuatia tukio hilo .

 
Msemaji wa jeshi la polisi nchini Advela Senso amesema tukio hilo limetokea wakati watoto wawili wakicheza ambapo mtoto mmoja alimwambia mwenzake kuwa akifanya jambo lolote baya dhidi ya Qur’uan atabadilika na kuwa nyoka.


Baada ya mtoto huyo kudaiwa kudhalilisha Quruan alianza kutafutwa na wazazi huku wazazi wa mtoto husika wakimbiza katika kituo cha polisi kwa ajili ya usalama.


Picha Mojawapo ya makanisa yanayodaiwa kuharibiwa likiungua moto.


Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Bw Said Meck Sadick amewataka wakazi wa jiji la Dar es salaam kuwa na subira kwa wakati huu ambapo vyombo vya dola vinaendelea kulishughulikia suala hilo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad