Akitoa
ufafanuzi wa kesi hiyo Kaimu Wakili wa Serikali Mfawidhi Athuman Matuma Kirati alisema kuwa ushaidi wa kesi hiyo umekamilika
kwa asilimia 100% na ofisi yake inaendelea na utaratibu wa kufungua jarada la
kesi hiyo Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba ambapo alisema kuwa leo mchana Septemba
3, 2018 jarada la kesi hiyo litaweza kufunguliwa katika Mahakama Kuu.
Wakili wa
Serikali Matuma alisema kuwa katika
kesi hiyo ya mauji Namba 18 ya mwaka 2018 kulingana na ushahidi uliokusanywa na
kukamilika kwa asilimia 100% unaonesha kuwa mauaji ya Mwanafunzi Sperius
Eradius yalikuwa ni mauaji ya kukusudia kutokana na silaha alizoshambuliwa nazo
mwanafunzi huyo.
|
Pamoja na
ushahidi huo lakini Wakili wa Serikali Matuma alieleza kuwa baadhi ya Walimu
walimwendea Mwl Respicius Mtazangira
kumuomba aache kumpiga mwanafunzi huyo lakini aliendelea kumpiga jambo ambalo
linaonesha alikusudia kumuua mwanafunzi Sperius
Eradius.
Marehemu Sperius Eradius alifariki dunia Agosti
27, 2018 muda mchache baada ya kupigwa shuleni Kibeta na Mwl Respicius Patrick Mtazangira aliyekuwa Mwalimu wa nidhamu
katika shule hiyo kwa kutuhumiwa kuiba mkoba (pochi) ya Mwl Herieth Gerald.
|
No comments:
Post a Comment