Mshauri wa
maswala ya Jinsia na Mafunzo katika mradi huo Bw. Paschal Tekwi amevitaka vikundi vya Ujarisiamali kuongeza
jitihada zaidi katika kuzalisha zao la muhogo ili vikundi hivyo viweze kupatiwa
mashine za kuchakata zao la muhogo na kutafutiwa masoko ya bidhaa hiyo ili
waweze kujiinuka kiuchumi.
|
Katika
kuendeleza kikundi hicho kinayo mikakati mbali mbali kinayotarajia
kufanya katika msimu ujao ikiwemo kulima kwa kutumia pembejeo za kilimo ili
kupata tija na faida kwa kuongeza thamani ya mazao na wingi wa mazao hali
itakayosaidia upatikanaji wa malighafi za kutosha.
|
Iwapo
kikundi hicho kitaona kuwa mradi huo wa mashine ya kuchakata zao la muhogo
unafaida basi watalipia asilimia 15 za gharama ya mashine hiyo na fedha
inayobaki watalipia ndani ya miezi 24 baada ya kukabidhiwa ili waweze
kuendeleza viwanda vidogo vidogo na hatimae kukuza uchumi wa kikundi chao na
wana kikundi kwa ujumla.
|
No comments:
Post a Comment