Wananchi wa Rutoro wakitoa malalamiko yao kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera walidai kuwa wanashindwa kuendeleza maeneo yao ya kilimo kutokana na Serikali kutomaliza mgogogro kati yao na Wawekezaji ambao ni wafugaji na mgogoro huo umedumu kwa takribani miaka kumi na miwili toka mwaka 2006 hadi sasa. |
Baada ya
kusikiliza malalamiko hayo kutoka kwa Wananchi na kutembelea Vitalu vya
Wawekezaji ambao ni Wafugaji, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Marco Gaguti aliwaeleza Wananchi wa Rutoro
pamoja na Wawekezaji kuwa alikwenda maeneo hayo kujifunza, kuona na kusikia
mwenyewe juu ya mgogoro huo ili autafutie ufumbuzi wa haraka ili kila upande
uendelee na shughuli zake za kulijenga taifa.
Katika hatua
nyingine Meneja wa Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) Mkoani Kagera Bw. Mashaka
Mlonge alimweleza Mkuu wa Mkoa kuwa NARCO sasa inafanya tathimini upya kuona
wawekezaji ambao hawajawekeza na kuviendeleza vitalu vyao kama walivyokubaliana
na Serikali ambapo tayari Vitalu vitano kati ya 54 vilivyopo Mkoani Kagera
Wawekezaji wake wamepewa “notice” ya kuachia vitalu hivyo.
|
No comments:
Post a Comment