Ushuhuda huo ulitolewa na akina mama wazazi katika wodi ya wazazi
kituoni hapo mara baada ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E.
Gaguti kufika kituoni hapo Septemba 7, 2018 kutembelea na kukagua ubora wa
majengo yaliyojengwa lakini pia thamani ya fedha za Serikali katika
ujenzi huo.
Kwa niaba ya akina mama wazazi waliokuwa wamepumzishwa katika wodi ya
wazazi mara baada ya kujifungua vichanga vyao Bi Schola Elias (30)
alimweleza Mkuu wa Mkoa wa Kagera, kuwa wanafurahia huduma za kituo hicho kwa
kuboreka baada ya Serikali kuleta fedha za kujenga majengo mapya hasa chumba
cha kujifungulia akina mama wajawazito na wodi ya wazazi pamoja na ukarabati
majengo ya zamani.
|
Ziara ya Mkuu huyo wa Mkoa wa Kagera katika kituo hicho cha Nyakanazi
wilayani Biharamulo imefanyika Septemba 7, 2018 na hadi Mkuu wa Mkoa Gaguti
alipowasili katika Kituo hicho majira ya saa 8:00 mchana walikuwa wamejifungua
akina mama tisa watoto wa kike wakiwa sita na wa kiume wakiwa watatu.
Katika hatua nyingine Bi Pili Ndamulo, Afisa Muuguzi Msaidizi ambaye ni
Msimamizi wa wodi ya wazazi katika Kituo hicho alisema kuwa wastani kwa wiki
wanajifungua akina mama 30 hadi 40 na kwa mwezi ni akina mama 100 hadi 120.
|
Naye Mkuu wa Mkoa Gaguti akiongea na wananchi katika Kituo cha Nyakanazi
mara baada ya kukikagua aliwataka wananchi hao kukitunza Kituo hicho, Pili
aliwataka watumishi katika kutoa huduma zinazoendana na ubora wa majengo ya
Kituo, Tatu wananchi kuchukua tahadhari ya ugonjwa wa EBOLA kwani Nyakanazi
inazo njia kuu mbili zinazoelekea nchi jirani za Burundi, Rwanda na Kongo DRC,
Mwisho aliwataka wananchi wote kujiunga na bima ya afya kwajili ya matibabu
yao.
Majengo yaliyojengwa katika Kituo cha Afya Nyakanazi ni pamoja na Wodi
ya Watoto, Wodi ya Akina Mama Wazazi, Nyumba ya Watumishi wawili, Chumba cha
kuhifdhia maiti, Jengo la kujifungulia, Njia za kutembelea na Kichomea
taka.
Aidha, majengo yaliyokarabaitiwa ni pamoja na Jengo la wagojwa wa nje,
Jengo la upasuaji na Mahabara.
Ujenzi huo umefanyika kwa jumla ya zaidi ya
shilingi milioni 566 fedha hizo zikijumuisha fedha za Serikali Kuu, Halmashauri
ya Wilaya pamoja na Wananchi wa Nyakanazi.
|
No comments:
Post a Comment