![]() |
Gor Mahia wanaenda fainali hiyo baada ya ushindi
wa bao 2-0 dhidi ya Singida United
katika mchezo nusu fainali ya pili leo June 7, 2018 Uwanja wa Afraha,kwa mabao ya Meddie
Kagere.
Simba SC nao wameenda fainali kwa ushindi wa penalti
5-4 dhidi ya Kakamega Homeboyz baada
ya sare ya 0-0 ndani ya dakika 90.
|
![]() |
Kikosi cha Simba SC.
Katika mashindano
hayo Simba SC ilipenya kwa penati
3-2 baada ya sare ya 0-0 pia dhidi ya Kariobangi
Sharks kabla ya kuendeleza ushindi wa staili hiyo mbele ya Kakamega iliyowatoa Yanga SC ya Tanzania pia kwa
kuwachapa 3-1.
Fainali ya michuano ya SportPesa Super Cup 2018 itafanyika Jumapili na mshindi pamoja na kupata dola za Kimarekani 30,000 pia atapata nafasi ya kwenda kucheza na klabu ya Everton Uwanja wa Goodison Park mjini Liverpool, England. Mshindi wa pili atajipatia dola za Kimarekani 10,000, wa tatu dola 7, 500 na wa nne dola 5,000 wakati timu nyingine zitapewa kifuta jasho cha dola 2,500. Bingwa mtetezi ni Gor Mahia ambayo mwaka jana iliifunga AFC Leopards 2-1 katika fainali uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. |
No comments:
Post a Comment