Uchafu huu wa Choo na Hatari ya Afya za Wafanyabiashara Soko la Nyankumbu Geita. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, May 23, 2018

Uchafu huu wa Choo na Hatari ya Afya za Wafanyabiashara Soko la Nyankumbu Geita.

Uchafu wa choo hicho.

Baadhi ya Wafanyabiashara katika Soko la Nyankumbu mkoa wa Geita wako hatarini kukumbwa na Magonjwa ya mlipuko kutokana na Choo cha soko hilo kujaa na kutiririsha maji kwenye bwawa linalotumika kuoshea bidhaa zao hasa mboga mboga na viazi.


Wakizungumza na Radio Kwizera sokoni hapo, baadhi ya wafanyabiashara Bi Lidia Deus na Devota Afready wamesema kutokana na harufu mbaya inayotokana na choo hicho imeathiri biashara zao za migahawa kutokana na wateja wao kuhofia kupata magonjwa ya mlipuko.
Pia wameiomba Serikali kuwarekebishia miundombinu ya choo hicho ili kuepuka magonjwa ya mlipuko ambayo yanaweza kujitokeza na kusababisha kufungiwa kwa biashara zao.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Geita Bw. Modest Aprinali amesema Serikali ipo kwenye mchakato wa kupunguza uchafu katika soko hilo na kwamba jitihada za haraka zinafanyika katika kuchimba shimo jingine kutokana na shimo hilo kujengwa kwenye mkondo wa maji hali inayosababisha kujaaa kwa haraka pale mvua inaponyesha.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad