NA WAMJW-DAR
ES SALAAM.
Naibu Waziri
wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amethibitisha kuwa hakuna mtu
aliyethibitika kuwa na ugonjwa wa EBOLA hapa nchini wala hakuna ugonjwa huo
hapa Tanzania.
Hayo
ameyasema leo jijini Dar es salaam mbele ya waandishi wa habari wakati akitoa
tamko kuhusu ugonjwa wa EBOLA kama ilivyodaiwa na baadhi ya vyombo vya habari
kuwepo kwa ugonjwa huo hapa nchini.
“Napenda
kuwatoa hofu watanzania kwamba hakuna ugonjwa wa EBOLA na wala hakuna mtu
aliyethibitika kuwa na ugonjwa huo, hivyo tuendelee na shughuli za kujenga
Taifa ila tunatakiwa tuchukue tahadhari za kujikinga juu ya ugonjwa huu”
alisema Dkt. Ndugulile.
Aidha, Dkt. Ndugulile amesema kuwa katika
kuchukua tahadhari juu ya ugonjwa wa EBOLA usiingie nchini Serikali imeweka
vifaa vya kupima joto la mwili (themo scaner) pia wapo wataalamu wa Afya
ambao wanauliza hali ya wageni
wanaoingia katika mipaka yote inayoizunguka nchi yetu ili kuzuia ugonjwa huo
kuingia.
Dkt. Ndugulile amesisitiza kuwa, Serikali haijafunga
mipaka ya nchi kwa sababu ya kujikinga na EBOLA.
“Tanzania
hatujafunga mipaka na hatuwezi kufunga biashara za mipakani ila tumeimarisha
ufuatiliaji wa watu wanaoingia nchini hususani maeneo ya viwanja vya ndege na
mipaka mingine yote.”
Mbali na
hayo Dkt. Ndugulile ameitaka mikoa
yote iliyo mipakani kudhibiti watu wote wanaoingia nchini kwa njia za panya ili
kuepusha uingizaji wa ugonjwa huo kwa wananchi
huku akiwataka wafanyabiashara wa mipakani kutoa ushirikiano ili kudhibiti
ugonjwa huo usiingie nchini.
Kwa upande
wake Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani ambaye pia ni Afisa wa kushughulikia
magonjwa ya kuambukiza Dkt. Grace Saguti
amesema kuwa Wananchi wanatakiwa kupata elimu juu ya kujikinga na ugonjwa huo.
“Elimu
inahitajika ya kutosha kwa wananchi wote hasa katika kufichua wagonjwa wa Ebola
kama watagundulika hasa wanaotoka nje ya nchi ili kupata msaada kutoka kwa
watoa huduma za afya walio yao juu ya kujikinga na ugonjwa huo.
|
Wednesday, May 23, 2018
Hakuna Mtu aliyethibitika na Ugonjwa wa Ebola Tanzania.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment