Mvua kubwa
iliyonyesha usiku wa kuamkia Jana March 21,2018 katika eneo la Nyahua wilayani
Uyui Mkoani Tabora imesababisha kukatika kwa barabara kuu ya Tabora kupitia
Itigi hadi Dodoma na kusababisha magari ya abiria na mizigo kwishindwa
kuendelea na safari zake kwa kutumia barabara hiyo.
Eneo la
barabara lilikatika liko umbali wa Kilometa 79 kutoka Tabora Mjini.
Akizungumza
na waandishi wa habari katika eneo la tukio Meneja wa Wakala wa Barabara
)TANROADS) Mkoa wa Tabora Mhandisi
Damian Ndabalinze alisema mvua zilizonyesha katika maeneo hayo zimesababisha
kukatika kwa eneo hilo ambapo ndipo barabara ya lami inaishia.
Aliwataka
madereva wa magari ya aina yoyote kuwa na subira kwa kutopita katika eneo hilo
kwa sababu wanaweza kuhatarisha maisha yao na abiria na mizigo.
Alisema
wakati taratibu nyingine zikiendelea za kutaka kurejesha mawasiliano kwa
kutumia barabara hiyo ni vema magari yote ya kuja na kutoka Tabora yakapitia
barabara ya Manyoni , Singida , Nzega hadi Tabora.
|
Naye Kamanda
wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoani Tabora SP Emilian Kamuhanda alisema wamejipanga kutoka
matangazo katika Stendi kuu ya mabasi Tabora na kushirikiana na Kikosi ya
Usalama Barabara cha Mkoa wa Singida ili kuwaelekeza madereva wote wapiti njia
ya Nzega ili kuepuka usumbufu.
Kwa upande
wa Mtendaji wa Kata ya Kizenge Maganga Saulo alisema mvua iliyonyesha usiku wa
kuamkia leo ilikuwa kubwa na kusababisha kukatika kwa eneo hilo , hatua
iliyopelekea magari kushindwa kupita.
Alisema ili
kuhakikisha hakuna maafa yatakayotokea wanatumia Jeshi la Akiba kuwazuia
madereva wanaotaka kujaribu kuvuka.
|
Baadhi ya
wasafiri kutoka katika Basi la Prince Ramigo na wakazi wa Nyahua wilayani Uyui
wakijaribu kuvuka Jana March 21,2018 katika eneo ambalo barabara imekatika kutoka na mvua
zinazoendelea kunyesha na kusababisha kukatika kwa mawasiliano baina ya Itigi
na Tabora. Nyuma ni basi dogo la Prince
Ramigo linalofanya safari zake kutoka Tabora kwenda Dodoma kupitia
Itigi.
|
No comments:
Post a Comment