Ushindi wa
Yanga SC 3-1 dhidi ya Stand United umeipa Yanga pointi tatu ambazo zinaifanya
ifikishe pointi 46 na kuifikia Simba SC licha kwamba wekundu wa Msimbazi
wanaendelea kuongoza ligi kwa tofauti ya magoli.
Magoli ya
Yanga yamefungwa na Ally Ally (alijifunga) dakika ya saba, Ibrahim Ajibu
akafunga goli la pili dakika tano baadaye, Obrey Chirwa ameifungia Yanga SC bao
lililokamilisha ushindi wa Yanga . Goli pekee la Stand United limefungwa na
Mayanga dakika ya 83.
|
Aidha kikosi
cha Yanga SC kimeondoka usiku wa jana March 12, 2018 kuelekea Gaborone,
Botswana, kwa ajili ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Township
Rollers FC.
Yanga SC imeondoka
na msafara wa wachezaji 20 pamoja na viongozi 11 kuelekea Botswana ambapo
mchezo huo utapigwa Machi 17 2018.
Katika mechi
ya awali iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Yanga SC ilikubali kichapo cha
mabao 2-1, hivyo sasa watalazimika kushinda zaidi ya mabao mawili, iwe 2-0, 3-0
au 4-1 ndiyo wataweza kusonga mbele.
|
No comments:
Post a Comment