Rais Weah
alipokuwa anakula kiapo mjini Monrovia.
Nyota wa zamani wa Soka Duniani, George Opong Weah ameapishwa kuwa rais
wa Liberia katika sherehe January 22, 2018 iliyohudhuriwa na maelfu ya watu katika mji
mkuu Monrovia.
Weah amechukua nafasi ya rais wa kwanza mwanamke kuwahi kuchaguliwa
kuongoza taifa la Afrika Bi.Ellen Johnson Sirleaf, ambaye amestaafu.
Kuingia kwa Weah madarakani kunakamilisha shughuli ya kwanza ya amani ya
mpito nchini humo tangu mwaka 1944.
Sherehe hiyo imehudhuriwa na viongozi wa mataifa kadha pamoja na nyota wa
kandanda duniani.
Akihutubia
baada ya kula kiapo, Weah amesema: “Nimekuwa katika viwanja vingi maishani,
lakini sijawahi kuhisi hivi.”
“Nitafanya
zaidi ya mchango ninaotarajiwa kutoa ili kutimiza matarajio yenu, lakini naomba
nanyi mtimize matarajio yangu, siwezi kutimiza haya peke yangu.”– George Weah
|
No comments:
Post a Comment