Jambo Bukoba
ni Shirika lisilokuwa la Serikali linalofanya kazi mkoani Kagera kwa
kushirikiana na serikali ya Mkoa.
Jambo
Bukoba ilianzishwa Mkoani Kagera kwa kusaidia watoto hasa Wanafunzi wa Shule za
Msingi kuanzia miaka 5 hadi 19 kujenga Afya zao Kimichezo ili kujikinga na
Maabukizi ya UKIMWI, kuweka haki sawa katika Elimu kupitia michezo kwa Wasichana
na Wavulana.
Tangu kuanzishwa
kwake mkoani Kagera limekuwa likiwafunza watoto katika shule za msingi kila
wilaya michezo midogo midogo ya kujenga ushirikiano wa pamoja hasa watoto wa
kike kujiamini na kushirikiana zaidi na wenzao wa kiume.
|
Wanafunzi
hao wa Shule ya Msingi Kigina,walicheza pamoja na kufundishwa michezo ya Pasi
Kumi,Tushikane Mabega,Tuvutane Kiuno,
Kiti Kisichokuwa na Mwisho na Mpira Huru.
|
Mwalimu wao wa Michezo –Mwl.Mwandu
Joseph Kusigwa akiwafundisha Wanafunzi
wake wa Shule ya Msingi Kigina,kucheza mchezo wa Kiti Kisichokuwa na Mwisho.
|
Wanafunzi
hao wa Shule ya Msingi Kigina,walicheza mchezo wa Mpira Huru.
|
No comments:
Post a Comment