Ligi ya
Wanawake ya Serengeti Premier Lite hatua ya nane bora inatarajia kuanza kutimua
vumbi Februari 24, 2018 kwenye viwanja vinne.
Mchezo kati
ya Kigoma FC na Simba Queens utakaochezwa kwenye uwanja wa Lake Tanganyika ndio
utakuwa mchezo rasmi wa ufunguzi.
Mechi
nyingine zitakazochezwa katika siku hiyo ya ufunguzi ni Panama watakaokuwa
nyumbani Uwanja wa Samora kucheza na Evergreen,JKT Queens wakicheza dhidi ya
Alliance kwenye uwanja wa Mbweni.
Mechi
nyingine ni ile itakayowakutanisha Baobab na Mlandizi Queens itakayochezwa
kwenye uwanja wa Jamhuri Dodoma.
Kabla ya
kufika kwenye hatua hiyo,ligi hiyo inayodhaminiwa na bia ya Serengeti Premier
Lite kinywaji murua na chenye ubora wa juu ilianzia kwenye hatua ya makundi
ikichezwa kwenye Kituo cha Dar Es Salaam kilichotumia Uwanja wa Karume na Kituo
cha Arusha kilichotumia Uwanja wa General Tyre.
|
No comments:
Post a Comment