
![]() |
Dr Sebuyoya
amewataja waliojeruhiwa kuwa ni Juma Samo (25) Joseph Otieno (30), Oscar Leonard
Sebastian (27), Baseke Mashinga Nyabashiki (31), Mahalulo Charles (25) na
majeruhi wa sita hajafahamika kwa kuwa hajajitambua na kwamba maiti waliofia
eneo la tukio ni Tisa na wawili wamefariki baada ya kufikishwa hospitalini
hapo.
Awali Mwenyekiti wa kijiji cha Mugera Bw Mapunda Kayuki amesema ajali hiyo imetokea jana January 14, 2018 majira ya Saa 11 jioni ambapo gari la Abiria aina ya Hiace lilitaka kukwepana na roli kwenye barabara ya Nyakanazi-Kahama kwenye kijiji hicho na kugongana ambapo dereva wa Hiace na Konda wake ni miongoni mwa waliofariki. Hiace hiyo yenye namba za usajili T 542 DKE ilikuwa ikitokea Kibondo kwenda Kahama ambapo maroli yaliyohusika kwenye ajali hiyo ni T 860 CGS, T 103 DUJ na T 147 DUJ ambapo magari yako chini ya usalama wa jeshi la polisi kwa uchunguzi zaidi. |
No comments:
Post a Comment