Paul amesema
majeruhi wengine sita wamepata matibabu na kuruhusiwa ambapo mwili wa marehemu
mwingine aliyepoteza maisha katika ajali ya kwanza iliyotokea kata ya
Nyantakara jumapili January 14,2018 haujatambulika na marehemu huyo wa jinsia
ya kike anakadiriwa kuwa na miaka zaidi ya 70.
Amesema pia
katika ajali hiyo iliyohusisha vifo vya watu 11 marehemu 10 walitambuliwa na
ndugu na miili ilichukuliwa kwa ajili ya mazishi na kati ya majeruhi watano
mmoja alisafirishwa hadi Hospitali ya Bugando kwa matibabu zaidi na wengine
walikwenda kutibiwa karibu na majumbani mwao kwenye maeneo walikotokea.
|
Kamanda wa Jeshi
la Polisi mkoani Kagera, Agustino Olomi amesema marehemu Sabina Daudi Kimoli
alipata ajali katika basi la Saratoga lenye namba za usajili T. 114 AAG
iliyokuwa ikitokea Mwanza kwenda Kigoma.
Amesema basi
hilo liligongana na roli lenye namba za usajili T803 BHQ na tela lenye namba T
281BGQ na kwamba madereva wa magari hayo wanashikiriwa na Jeshi la Polisi kwa
upeleleza zaidi kabla ya kufikishwa kwenye mkondo wa sheria.
|
No comments:
Post a Comment