Wahitimu
waliweza kushiriki katika kuanzisha miradi ya ujasiliamali , michezo, na
kushiriki malezi ya kiroho bila kujali tofauti za madhehebu yao na hii ni
mipango ya ufanisi wa shule hiyo.
Shule inayo
miradi ya kilimo na ufugaji kwa kuwapatia elimu ya kujitegemea na mafunzo ya
kutengeneza bidhaa mbalimbali ili wanapohitimu elimu ya sekondari waweze
kujikwamua kiuchumi.
|
Mojawapo ya
miradi yenye kufurahisha walimu na wanafunzi kwa wiki mbili zilizopita wakiwemo
wafanyakazi ni kupatikana kuchimbwa kwa kisima cha maji ambayo ni moja ya
changamoto ya muda mrefu ambapo kero ya pili ilikuwa ni umeme ambao umefungwa
na REA utakaoingia hadi chanzo cha maji ya mto Mpanyura
Changamoto.
Upungufu wa
vyumba vya madarasa na baadhi ya majengo kuchakaa baada yakuongezeka kitengo
cha taasusi ya sayansi na visima vya kuvuna maji ya mvua hivyo waliowahi
kusomea katika shule hiyo kutumia elimu na mapato yao kusaidia kuboresha
miundombinu iliyokuwa ikitumika kuwainua kitaaluma.
Wosia kwa
Wahitimu.
Kuhakikisha
wanatumia elimu na malezi kudumisha nidhamu na maadili mema kwenye jamii
watakapokuwa wakitoa huduma mbalimbali kupitia vipaji na fani watakazoendelea
kupata ndani na nne ya nchi.
Baadhi ya
wanafunzi wa shule hiyo waliohitimu na wanaoendelea na masomo wameupongeza
uongozi wa shule hiyo kwa kuwapatia kisima cha maji kuwaondolea kero ya maji ya
muda mrefu kwa kuvunja ratiba ya kufuata
maji mto Mpanyula na sasa wanaomba gari la kusafria
|
Mgeni rasmi, Mbunge wa Jimbo la Ngara mkoani Kagera, Alex Gashaza
aliyewakilishwa na Afisa Elimu Idara ya
Msingi kitengo cha Elimu ya watu wazima
Bw Frank Kitunzi ambaye amesema Wahitimu hawana budi kufanya
shughuli za kusaidia wazazi na jamii inayowazunguka ikiwa ni pamoja na kutunza mazingira pia kushiriki
matukio ya kijamii kuleta hamasa ya
kuwaendeleza kitaaluma.
Pia amesema
kujihadhari na maadili mabaya kwa kutumia madawa ya kulevya ya aina mbalimbali
na kujihadhari kuendesha vyombo vya moto bila kuzingatia sheria za usalama
barabarani na katika maisha yao kufunga nadhiri na pingu za ndoa takatifu kwa
kuepuka anasa zinazomchukiza mungu.
Kwa upande
wa wazazi kuendelea kutoa malezi ya kiroho , kwa mila na desturi kufuata
tamaduni halali za kitanzania na afrika kuelekea uchumi wa kati na wa viwanda
|
Katika
mahafali hayo Mbunge Alex Gashaza ameahidi Shilingi laki tano
kuweza kupunguza changamoto za shule hiyo hasa kununua vifaa vya ujenzi wa
chumba cha darasa kwa ajili ya kufundishia masomo ya sayansi kwa vitendo.
|
No comments:
Post a Comment