Taswira Picha Mgogoro wa Ardhi Karagwe Unavyochukua sura Nyingine. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, September 05, 2017

Taswira Picha Mgogoro wa Ardhi Karagwe Unavyochukua sura Nyingine.

Tarehe 30-31.8.2017 ZAIDI YA KAYA 91 KIJIJI CHA KANOGO NA CHABUHORA WILAYA YA KARAGWE Mkoani Kagera, waachwa BILA MAKAZI, bila chakula na katika mahangaiko makubwa.. Wahanga wanahitaji msaada wa haraka. 

Nyumba zao zimechomwa moto na zingine kuharibiwa huku mashamba yakikatwa kuwalazimisha kuondoka eneo hilo wanalodai walipewa na serikali ya kijiji!! inadaiwa wamevamia vyanzo vya maji. Wao wanadai mgogoro unatokana na wenye mifugo waliovamia eneo hilo na sasa wanasabisha kero hiyo.

NB:, serikali ya wilaya Mko wapi? Tusaidieni Majibu ya suala hili Kabla Halijawa kubwa zaidi ya lilivyo kwa sasa Ikumbukwe hili sio tatizo la kuchukuliwa kikawaida ni tatizo kubwa Sana'a ,Migogoro kati ya wafugaji na Wakulima, haitakiwi kutatuliwa kwa Mabavu kama inavyosadikika ......,,,,Migogoro kama hii inatakiwa kutatuliwa kwa Weledi Mkubwa zaidi , Hekima pamoja na busara havinabudi kutumika Vinginevyo Kuna MTU atajikuta anakuwa Mwendelezaji wa Migogoro badala ya kuwa Mtatuzi


Hawa wanadaiwa wamevamia vyanzo vya maji !! Inadaiwa na viongozi pia kuwa hili ni eneo la wafugaji !! Serikali ya kijiji iliwapa ardhi kaya zile waishi na walime. Wanazo stakabadhi! Ipo sintofahamu hapo,

Msaada wa hali na mali ikiwemo wa kisaikolojia unahitajika kwa waathirika wa tukio hili hususani akina mama, watoto,, na wanachi wote kwa ujumla ambao kwa sasa, wanashindwa waende wapi au wafanye nini. Mvua za masika zimeanza na wananchi hawa hawana pa kulala.. na hawana chakula....





Tukio hili linakuja sasa kufuatia Mkuu wa Wilaya Karagwe ,Bw.Godfrey Mheruka kuanzisha operation ya kuondoa wavamizi wa vyanzo vya maji na uchafuzi wa mazingira.






DC Mheruka akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wilaya hiyo, ameanzisha operation hiyo ya kuondoa wananchi waliovamia katika vyanzo vya maji na kuharibu mazingira ambapo wakiwa katika kijiji cha Chabuhora katika Kata ya Nyakabanga, waliwakuta  wananchi wanaodaiwa kuvamia vyanzo vya maji na kuweka makazi na kuanzisha shughuli za kibinadamu ikiwemo kilimo, kukata miti hovyo, kuchoma mkaa pamoja na uwindaji haramu.

Aidha waliamua kuteketeza makazi ya wananchi hao na kuwataka warudi katika makazi yao ya zamani ikiwa ni pamoja na kuwaagiza Watendaji wa Kitongoji hadi Wilaya kusimamia zoezi hilo kuhakikisha hawarudi katika maeneo hayo kabla hatua kali za kisheria hazijachukuliwa dhidi yao.





Habari/Picha Na Joseph Sekiku.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad