Simon Msuva pichani
amesema magoli mawili aliyofunga kwenye mechi dhidi ya Botswana yatamsaidia
kujiamini katika klabu yake ya Difaa El Jadid pindi atakaporejea Morocco.
Msuva
amecheza katika kiwango cha juu dhidi ya Botswana na kufanikiwa kutumia vizuri
nafasi alizozipatakupachika mabao yaliyoipa Taifa Stars ushindi wa magoli 2-0 kwenye
uwanja wa nyumbani.
“Magoli
mawili niliyofunga kwenye timu ya taifa yataniongezea kujiamini na kwenda
kufanya vizuri kwenye klabu yangu lakini nitaendelea kuaminika kwenye timu kwa
sababu unapocheza kwenye timu ya taifa na kufunga wanaona huyu mchezaji anaweza
kutusaidia,” Simon Msuva.
|
Taifa Stars ilipata ushindi wa magoli 2-0 mwezi March 25, 2017 katika ushindi ambao imeupata tena leo
Septmber 2, 2017 yote ikiwa ni michezo ya kirafiki ndani ya miezi saba.
|
No comments:
Post a Comment