“Nimeonana na Mh. #TunduLissu katika chumba chake hospitali ya Nairobi na
kuzungumza naye kuhusu hali yake na anavyoendelea.UKWELI ni kwamba, ameumizwa
vibaya.
Imeelezwa kwamba MADAKTARI wanaendelea na hatua kadhaa za matibabu,
wakiwa wameanza kwa kumuimarisha (stabilization), ili kuufanya mwili uweze
kumudu hatua zaidi za utibabu anazopaswa kufanyiwa.
AIDHA, katika kuongea naye,
Mh. Lissu ameonesha uso wa tabasamu, huku akimshukuru MUNGU kwa kumruhusu
kuwepo hai.
NAAMINI kwamba hatua zaidi na za haraka zitahitajika kumsaidia apate huduma za kitabibu katika ubora na ufanisi uliopo kwa sasa duniani.“ameandika Mhe Lazaro Nyalandu kwenye ukurasa wake wa Facebook mapema jana baada ya kuonana na Lissu, huku akiwataka Watanzania kuendelea kumuombea apone haraka.
“Ni maombi yangu kwetu SOTE , tuweke pembeni tofauti zetu za kiitikadi,
ama mitazamo, tuungane na kushikamana kama Taifa kwa ajili ya kumwomba MUNGU
anyooshe mkono wake, na kumponya. HALIKADHALIKA, SOTE tuungane kutoa msaada wa
hali na mali kwa kadri ya uhitaji wake. AMANI iwe naye!“ameandika Lazaro
Nyalandu.
Mhe Tundu Lissu alipigwa risasi mnamo tarehe 7 Septemba 2017, Mjini
Dodoma katika eneo la Area D karibu na nyumbani kwake na watu wasiojulikana.
|
Sunday, September 17, 2017
Mhe Lazaro Nyalandu - '' Tuweke pembeni tofauti zetu, Tundu Lissu ameumizwa Vibaya ''
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment