Justine Charles akiwa amekamatwa na shehena ya Madawa ya kulevya aina ya Bangi magunia 37 huko nyumbani kwake Mkatokatoke kijiji cha Ntobeye wilayani Ngara mkoani Kagera tarehe 15,09,2017.
|
Jeshi la
Polisi wilayani Ngara mkoani Kagera linamshikilia Justine Charles
maarufu kama Sande mkazi wa kitongoji cha Matoketoke kata ya Ntobeye baada ya
kukutwa na gunia 57 za bangi sawa na kilogram elfu 2 na 75 zikiwa zimehifadhiwa
nyumbani kwake.
Akizungumza
na Radio Kwizera akiwa Makao Makuu ya Polisi Ngara, Kamanda wa Polisi mkoa wa
Kagera Augostine Ollomi amesema mafanikio ya kukamata bangi hiyo yamekuja
kufuatia oparesheni ya kutokomeza uhalifu iliyoanza Septemba 10 na kumalizika
Septemba 16 mwaka huu,2017 ikihusisha mikoa ya Kagera, Kigoma na Geita.
|
Akizungumza
akiwa kituoni hapo mtuhumiwa huyo Justine Charles -Pichani amesema licha ya kuwa ulimaji
wa bangi ulipigwa marufuku na serikali lakini aliamua kuendelea kulima kutokana
na ugumu wa maisha alionao ili ajipatie kipato.
Kamanda
Ollomi amesema katika oparesheni hiyo iliyofanyika maeneo mbalimbali ya mkoa wa
Kagera pia wamefanikiwa kukamata kilogram 10 za mirungi, lita 527 za pombe aina
ya Gongo, watu 25 wanaojihusisha na wizi, piki piki mbili, Ng’ombe 16 waliokuwa wakisafirishwa pamoja na
raia 60 wa kigeni walioingia nchini bila kufuata utaratibu.
|
No comments:
Post a Comment