Simba SC wakiwa Bukoba.
Kesho;Jumapili
April 02,2017 zipo Mechi 4 na Macho Kodo ni huko Uwanja wa Kaitaba Mjini Bukoba
kati ya Kagera Sugar, walio nafasi ya 4, wakiwavaa Vinara Simba SC.
Mbio za Ubingwa
zinaongozwa na Wekundu wa Msimbazi, Simba SC wenye pointi 55, wakifuatiwa na
watetezi wa taji, Yanga SC wenye pointi 53 baada ya timu zote kucheza mechi 24
na wikiendi hii miamba hiyo ya soka nchini itamenyana na timu zinazowafuatia
kwa ubora katika Ligi Kuu, Azam FC inayoshika nafasi ya tatu kwa pointi zake 44
na Kagera Sugar iliyo nafasi ya nne kwa pointi zake 42, kufuatia kila timu
kucheza mechi 24.
Msimamo VPL 2016/2017.
|
Mechi nyingine
za Jumapili ni Jijini Dar es Salaam kati ya African Lyon na Stand United, Mjini
Mbeya ni Tanzania Prisons na Mtibwa Sugar na huko Mwadui Complex, Shinyanga ni
Mwadui FC na JKT Ruvu.
VPL – LIGI
KUU VODACOM
Jumamosi
Aprili 01,2017.
Yanga SC v
Azam FC
Maji Maji FC
v Toto Africans
Mbeya City v
Ruvu Shooting
Jumapili
Aprili 02,2017.
Kagera Sugar
v Simba SC
African Lyon
v Stand United
Tanzania
Prisons v Mtibwa Sugar
Mwadui FC v
JKT Ruvu
|
No comments:
Post a Comment