Aidha mbunge
huyo amesema kuwa yupo kwenye harakati za kukamilisha kukiandika kitabu chake
kitakachotoka hivi karibuni chenye historia ya maisha halisi ya wafungwa
waliopo gerezani bila hatia,sambamba na wale waliobambikiziwa kesi mbalimbali.
Amewataka
madiwani kuwa sambamba na yeye na kuachana na kauli wanayoisema ya kuwa wapo
nyuma yake kwa kila kitu anachokifanya .
|
Mamia ya
wananchi waliohudhuria katika mkutano huo leo jijini Arusha.
|
Mbali na
Lema, mwingine aliyepata nafasi ya kuzungumza na umati huo uliojitokeza Jana ni
mwanachama mpya wa chama hicho, muigizaji Wema Sepetu.
Mkutano huo
umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama mkoani humo akiwemo Mstahiki Meya
wa Jiji la Arusha, Kalist Lazaro.
|
No comments:
Post a Comment