Mkuu wa mkoa
wa Dar es salaam Paul Makonda, leo February 8 2017 amesimama mbele ya Waandishi
wa habari kwenye awamu ya pili ya ishu ya dawa za kulevya na kutaja watu
mbalimbali wanaotakiwa kufika Polisi Ijumaa kwa ajili ya mahojiano kuhusu ishu
za dawa za kulevya.
Kabla ya
kuhitaja List hiyo ya wa tu 65, RC Makonda ameeleza njia 5 ambazo zinatumika na
wafanyabiashara wa dawa za kulevya, baada ya kufanya utafiti wake…….
1:- Watu
wananunua dawa kutoka Pakstani wanakuja na meli, meli inapakia mizigo, meli
ikishapaki mzigo wanachukua dawa za kulevya wanaingiza kwenye mifuko kama ya
sukari halafu wanapakia kwenye mapipa wanayaingiza kwenye meli, meli zinapokuja
zinapokaribia kwenye bandari zetu wanayatupa mapipa hayo yakiwa yamefungwa na
GPRS, maeneo wanayoyatupa mapipa hayo ni Zanzibar, Tanga na Bagamoyo.
wakishakuja kwenye bandari zetu hawana dawa za kulevya baadye timu inaenda
wakiwa na boti wakiwa na mashine zao za kusoma GPRS wananyanyua yale mapipa.
2:- Njia ya
magari, mtu ananunua magari Japan lakini hatoki moja kwa moja Japan kuja
Tanzania anapita nchi zingine kwa ajili kuweka mzigo, anafungua baadhi ya sehemu a magari wanaweka
dawa za kulevya.
3:- Watu
wanafanyabiashara kwenye meli za mafuta, sisi huwa tu tunaangalia mafuta kama
yana viwango sasa huwa wanatumia huo mfumo kusafirisha.
4:- Kuna watu wana sehemu zao za kupack boti zao
hawaingiliwi na mtu, anachokifanya anaenda kuchukua mzigo anasafirisha.
5:-Kuna
wanaotoa dawa za kulevya hapa kwa mfano kuna mama ambaye kazi yake ni
kusafirisha watoto wa kike anasema anaenda China kununua bidhaa, anasafirisha
watoto wa kike wenye umri wa kati, wanapewa dawa wanasafiri nazo wanapewa na
Dola 5000 akifanikiwa kuingiza analipwa dola 7,000.
|
No comments:
Post a Comment