Mkuu wa
wilaya ya Ngara Luteni Kanali Michael Mtenjele alisema katika msako wa kuwakamata
wakulima wa bangi wilayani Ngara jumla ya mashamba ekari 20 yalibainika na
wakulima wa zao hilo wanalilima katikati ya mapori wilayani humo
Mntenjele
alisema wakulima waliokamatwa na kuhojiwa walidai wanauz zao hilo kati ya
Sh15,000 hadi Sh 17 000 kwa wateja kutoka nchi jirani za Rwanda na Burundi na
kwamba wanalima zao hilo wakikata miti kwenye vyanzo vya maji
“Wanapolima
bangi wanaiweka katikati ya mashamba ya mahindi na huwezi kutambua kwani
wanatembea umbali mrefu katikati ya mabonde yanye vyanzo vya maji na kukata
miti kisha kupanda kupanda bangi hiyo”Alinema Kanali Mntenjele
Alisema
katika msako uliofanyika kwa siku tatu wilayani Ngara kata ya Ntobeye, Keza
kiasi cha ekari 20 zilibainika, wanaolima zao hilo wakiwatumia hata
wahamiaji haramu kutoka mataifa jirani na wilaya hiyo wakiishi porini na
kuletewa mahitaji ya chakula.
|
Aidha mkuu
wa wilaya ya Biharamulo Saada Malunde alisema kata iliyofanyiwa msako kukamata
wakulima wa bangi ni kata ya Nyantakara na Nemba ambapo mkulima mmoja James
Maliatabu (35) alikutwa na shamba la bangi ekari 10.
Alisema vita
ya dawa za kulevya kwa maeneo ya vijijini ni utumiaji wa bangi ambapo pia
kamati za mazingira katika vitego na idara za halmashauri zinatakiwa kuunga
mkono serikali kuwataja na kuwakamata wanaojihusiha na biashara ya madawa ya
kulevya ili kufikishwa kwenye vyombo vya sheria
Pia baadhi
ya wajumbe wa kamati za ulinzi na usalama katika wilaya hizo walishauri
serikali za vijiji na madiwani hata maafisa kata na tarafa kufanya zoezi la
kuwasaka wakulima wa bangi kila mahali ili kutokomeza madawa ya kulevya kote
nchini.
|
No comments:
Post a Comment