Ushindi huo
unakuja baada ya Cameroon kufumgwa fainali mbili za AFCON na Misri, walifungwa
fainali ya AFCON 2008 kwa kipigo cha goli 1-0 la Mohamed Aboutrika, lakini
mwaka 1986 walipoteza tena mchezo wa fainali.
Sasa
Cameroon wanakuwa wamechukua taji lao la tano la AFCON huku Misri bado
wakiendelea kuwa wababe wa taji hili wakiwa na rekodi ya kulichukua mara saba.
|
Misri ndio waliotangulia kufunga katika
Dakika ya 22 Mfungaji akiwa Kiungo wa Arsenal Mohamed Elneny na Bao hilo kudumu
hadi Haftaimu.
Kipindi cha
Pili, Wachezaji Wawili wa Cameroon walioanzia Benchi ndio waligeuza Mechi pale
Nicolas N’Koulou aliposawazisha Dakika ya 59 na Vincent Aboubakar kuwapa
ushindi Dakika ya 88.
Bao hizo
ziliamsha nderemo na vifijo miongoni mwa Mashabiki 38,000 wengi wao wakiwa ni
wa Cameroon.
|
NCHI
ZILIZOWAHI KUTWAA UBINGWA WA AFRIKA.
-Egypt-Mara
7
-Cameroon- Mara 5
-Ghana-Mara
4
-Nigeria-Mara 3 -Congo DR-Mara 2 -Zambia, Algeria, Congo, Ethiopia, Ivory Coast, Morocco, South Africa, Sudan, Tunisia-Mara 1 |
No comments:
Post a Comment