Watu Watatu wafariki Katika Ajali ya basi Mkoani Singida - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, January 09, 2017

Watu Watatu wafariki Katika Ajali ya basi Mkoani Singida

Matukio ya ajali za barabarani yameendelea kuutikisa Mkoa wa Singida baada ya abiria 10 kupoteza maisha na wengine zaidi ya 30 kujeruhiwa ndani ya siku tisa. 

Desemba 30, mwaka jana,2016 katika Kijiji cha Tumuli Wilaya ya Iramba abiria watatu walikufa na wengine 25 kujeruhiwa na ajali nyingine ilitokea Januari Mosi katika Kijiji cha Kintukuntu wilaya humo na kuua abiria mmoja na kujeruhi watatu. 

Ajali nyingine iliyohusisha bajaji ilitokea jana  Januari 7 katika Barabara ya Mwankoko na  kumuua dereva na abiria wawili. 

Siku moja kabla ya tukio hilo, ajali ya basi la Mohammed Trans lililokuwa linatokea Tanga kwenda Shinyanga ilisababisha vifo vya abiria watatu na kujeruhi wengine watano wote wakiwa ni walimu. 
Akitoa taarifa ya ajali ya basi la Mohammed Trans jana,January 08,2017, Kaimu Kamanda Polisi mkoani hapa, Mayala Towo alisema ilitokea Januari 6, saa nne usiku katika Kijiji cha Mseko wilayani Iramba. 

Kamanda huyo aliwataja waliofariki dunia kuwa ni Mussa Rajabu (55), Farahan Manyama (34) na John Tungaraza (39) wote wakiwa ni walimu, wakazi wa Geita. 

Pia, alisema majeruhi ambao pia ni walimu wamelazwa katika hospitali ya wilaya hiyo. 

Kamanda huyo aliongeza kuwa walimu hao walikuwa wametokea kwenye Chuo cha Eckenford mkoani Tanga walikokuwa wakichukua mafunzo mbalimbali. Alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva. 

Towo alisema basi hilo lenye namba za usajili T 786 AWJ aina ya Scania lilikuwa linaendeshwa na Jovin Jackson (38), mkazi wa Shinyanga liligonga kwa nyuma lori lenye namba B.6705A lililokuwa likivuta tela B.0568A lililokuwa likienda Burundi. 

Akifafanua, alisema dereva wa basi alitaka kulipitia lori hilo, lakini alipogundua hataweza aliamua kurudi ghafla kushoto na mwendo kasi aliokuwa nao alijikuta analigonga lori hilo kwa nyuma. 

Towo alisema baada ya kusababisha ajali hiyo dereva alitoroka na kukimbilia kusikojulikana. Juhudi zinaendelea kumsaka ili afikishwe mahakamani.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad