![]() |
|
Jacob Louis 'Kaparata'
akiingia kwenye gari lake alilolitengeneza mwenyewe kwa miezi mitatu.
|
![]() |
|
“Nilipokuwa mdogo
nilikuwa mtundu sana nikitengeneza magari na vitu mbalimbali kwa kuiga
nilivyoviona, ndipo watoto wenzangu wakanipachika jina la ‘Kaparata’, ambalo
nimelizowea na kuamua kuiita kampuni yangu kwa jina hilo.
“Tangu mdogo nilipenda
kuangalia filamu na nilivutiwa na gari moja nililoliona kwenye filamu ya Delta
Force ya Chuck Norris (The Flyer 72 Advanced Light Strike Vehicle) nikaapa
kwamba lazima nije nitengeneze gari la aina hiyo,” anasema Kaparata.
Hata hivyo, anasema
kwamba, alitumia muda wa wiki mbili kutengeneza chassis ambayo alihakikisha
inanyooka na kukaa sawa kabla ya kuendelea na utundu mwingine.
“Hivi sasa nikitembea
na gari yangu, hata kama tumeongozana na magari mengine ya kifahari, watu
wataitazama gari yangu mitaani na wamevutiwa nayo huku wengine wakinitaka
nitengeneze mengine niyauze,” anasema.
Anasema wakati anaanza
kuitengeneza gari hiyo vifaa pekee alivyokuwa navyo ni drill machine, grander
na welding machine – vifaa vitatu tu, ambapo mabati na vifaa vingine
alivinunua.
Kwa kuwa yeye si fundi
mchundo, mabati na vifaa vingine aliyapeleka kwa mafundi mchundo ambao
walimkunjia kwa muundo na vipimo alivyovitaka yeye.
“Lakini nimeingia
hasara kubwa kwa sababu wakati mwingine unampelekea mtu akukunjie bomba au
bati, lakini anakosea, inabidi kulitupa na kutafuta jingine.....BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI HABARI HII.
|














No comments:
Post a Comment