Makamu Mwenyekiti-Zanzibar Dkt Shein
akimpongeza Mwenyekiti Mpya,Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa kuteuliwa kuwa
mwenyekiti wa chama hicho kwa miaka 10,pichani katia anaeshuhudia ni Mwenyekiti
aliyemaliza muda wake Dkt Jakaya Kikwete.
|
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrhamani
Kinana akimpongeza Mwenyekiti Mpya,Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa kuteuliwa
kuwa mwenyekiti wa chama hicho kwa miaka 10.
|
Mwenyekiti
mpya wa chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli akihutubia mbele ya
Wajumbe wa Mkutano mkuu Maalum wa chama cha CCM mara baada ya kutangazwa rasmi
kuwa Mwenyekiti wa chama hicho.
Dkt. John
Pombe Magufuli ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anavunja
rekodi baada ya kutangazwa kuwa Mwenyekiti wa Chama Taifa kwa kupata asilimia
100 ya kura zote zilizopigwa.
Rekodi hiyo
ya kupata asilimia 100 ya kura zote kwenye uchaguzi wa aina hiyo (Uenyekiti wa
Chama Cha Mapinduzi Taifa) haijawahi kufikiwa na kiongozi yeyote ndani ya CCM
tangu kuanzishwa kwa chama hico Februari 05, 1977 ambapo ni miaka 39 sasa.
Wenyeviti wa
CCM waliyopita ambao ni Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Ali Hassan
Mwinyi, Benjamin William Mkapa wala Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
hawakuwahi kupata kura zote zilizopigwa kwenye uchaguzi wa ngazi hiyo.
|
No comments:
Post a Comment