Picha
juu na chini ni Baadhi ya mafundi wakijaribu kuchimba udongo katika eneo la mto
Lagosa ambako daraja hilo linajengwa.
|
Baadhi
ya malighafi zinazotumika kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo zikiwa eneo la ujenzi.
Na
Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii aliyeko Kigoma.
Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) limetoa Sh. Milioni 584 kwa ajili ya ujenzi wa
madaraja mawili ikiwa ni njia moja
ya kutatua changamoto ya miundombinu ya barabara katika vijiji vinavyopakana na
Hifadhi ya Taifa Milima ya Mahale vilivyopo wilaya ya Uvinza mkoani
Kigoma.
Baadhi
ya Wananchi wanaoishi katika vijiji vya Lukoma na Igalula wanakabiliwa na
changamoto ya barabara jambo linalowafanya washindwe kufanya shughuli zao za
kimaendeleo.
Akizungumza
na waandishi wa habari waliotembelea vijiji hivyo vilivyoko mwambao mwa zimwa Tanganyika,
Mkuu wa idara ya ujirani mwema ,Mhifadhi Romanus Mkonda aliyataja madaraja hayo
kuwa Lagosa na Lukoma.
“Daraja
la Lagosa linatumia Sh. Milioni 296 wakati lile la Lukoma litatumia Sh. Milioni
288,” alisema.
Alisema
lengo la TANAPA ni kusaidia jitihada za serikali za kuimarisha mawasiliano ya
barabara katika ukanda huo kwa ajili ya kuwawezesha wananchi kiuchumi.
Aliongeza
kuwa kwa mwaka wa fedha 2016/17, TANAPA imetenga Sh. Milioni 500 kwa ajili ya
kujenga madaraja ya Nkonkwa na Igalula yaliyopo vijijini hapo.
Naye
mwenyekiti wa kijiji cha Igalula, Mussa Matililo alisema iwapo madaraja hao
yatakamilika itawarahisishia wananchi wa maeneo hayo katika shughuli zao za
kilimo...SOMA ZAIDI KWA KUBOFYA HAPA.
|
No comments:
Post a Comment