EURO 2016:-Wenyeji Ufaransa waenda Robo Fainali, sasa watacheza na Mshindi kati ya Uingereza na Iceland. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, June 26, 2016

EURO 2016:-Wenyeji Ufaransa waenda Robo Fainali, sasa watacheza na Mshindi kati ya Uingereza na Iceland.

Mshambuliaji Antoine Griezmann kaifungia mabao yote mawili dakika za 57 na 61 Timu yake ya Taifa ya Ufaransa ilipo shinda  magoli 2-1 dhidi ya Jamhuri ya Ireland katika mchezo wa hatua ya 16 Bora Euro 2016 jioni ya leo,June 26, 2016 kwenye Uwanja wa Parc Olympique Lyonnais mjini Decines-Charpieu na Ufaransa kwenda Robo Fainali.


Ufaransa walisawazisha Dakika ya 57 kupitia Antoine Griezmann na Dakika 4 baadae Griezmann akapiga Bao la Pili.

Jamhuri ya Ireland walipata pigo jingine Dakika ya 66 pale Shane Duffy alipopewa Kadi Nyekundu kwa kumwangusha Griezmann aliekuwa akichanja mbuga kumwona Kipa.

Kwenye Robo Fainali, Ufaransa watacheza na Mshindi kati ya Uingereza na Iceland.


Jamhuri ya Ireland walianza vyema na kupata Penati Dakika ya Pili tu pale Kiungo wa France Paul Pogba alipomwangusha Shane Long ndani ya boksi na Mwamuzi Nicola Rizzoli wa Italy kutoa Penati iliyopigwa na Robbie Brady na kupiga Posti ya chini na kutinga wavuni.
Usiku huu,Ujerumani wanaongoza bao 3-0 dhidi ya  Slovakia huko Stade Pierre Mauroy, Lille na kisha baadae  Hungary dhidi ya Belgium huko Stadium de Toulouse Mjini Toulouse.

Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya EURO 2016 itamalizika Jumatatu,June 27, 2016 kwa Mechi mbili , ya kwanza ni kati ya Italia dhidi ya Mabingwa Watetezi Hispania itakayochezwa Stade de France, Paris wakati ya mwisho ipo Mjini Nice kati ya Uingereza na Iceland.

Washindi wa Raundi hii watatinga Robo Fainali ambazo Mechi zake zitaanza Alhamisi,June 30, 2016.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad