Kikosi cha Medeama ya
Ghana katika Picha ya Pamoja.
Klabu za Medeama ya
Ghana na MO Bejaia ya Algeria zimetoka suluhu ya bila kufungana katika mchezo
wa kundi A michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika.
Sare hiyo unawafanya
wawakilishi wa Tanzania Young Africans kushika nafasi ya mwisho katika kundi
hilo baada ya kupoteza michezo yake miwili ya awali walipofungwa na MO Bejaia
kwa bao 1 - 0 na kupokea kipigo cha idadi hiyo hiyo kutoka kwa
TP Mazembe ya DR Congo.
Yanga italazimika
kushinda mechi ijayo dhidi ya Medeama mchezo utakaopigwa Julai 15,2016 katika uwanja
wa Taifa siku ambayo MO Bejaia itakua inacheza na vinara wa kundi hilo TP
Mazembe.
Nayo Klabu ya soka ya
Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini imeifunga Enyimba ya Nigeria mabao 2 - 1 mjini
Pretoria katika mchezo wa ligi ya mabingwa barani Afrika siku moja baada ya
vigogo wengine wa Afrika Al Ahly kuambulia kichapo nyumbani dhidi ya Asec
Mimosas.
Kabla ya mchezo huo
Sundowns waliwafunga Entente Setif ya Algeria 2-0 lakini mchezo huo ukatangazwa
batili baada ya Setif kushindwa kuwazuia mashabiki wao kufanya fujo.
Ushindi huo unaipa
Sundowns alama sawa na Zamalek katika kundi B timu zote zikiwa na ushindi wa
mchezo mmoja huku zikiwa zimesalia timu tatu katika kundi hilo.
|
No comments:
Post a Comment