Getrude Clement ,Binti mwenye umri wa miaka 16 kutoka Jijini Mwanza,Nchini Tanzania
amehutubia mbele ya Viongozi mbalimbali wa Dunia kwenye hafla maalum ya Mkutano
wa Makubaliano ya Paris , Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa (UN), New York,
Marekani kama mwakilishi mtandao wa wanahabari watoto wa Shirika la Kuhudumia
Watoto Duniani, UNICEF.
Getrude alipata nafasi ya kuwakilisha Vijana kutoka Ulimwenguni kote
alipohutubia Baraza hilo akiwa mwenye kujiamini na kutoonekana kuwa na hofu
japo anaongea kwenye jukwaa ambalo linatazamwa na viongozi mbalimbali.
Mataifa zaidi ya 150 yalitia saini
makubaliano ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo Marekani ambapo
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,Bw. Ban
Ki Moon ndio alimkaribisha Getrude
kuongea kwa kusema ‘’…ni furaha yangu kumualika Getrude Clement ambaye pia ni
Mwakilishi wa Vijana anayeishi Tanzania na anaziwakilisha Sauti za Vijana‘
Iliripotiwa Maraisi 60 walihudhuria
na Getrude alianza kwa kuwasalimia
waalikwa kisha …’’alizungumzia
mabadiliko ya tabia nchi, hatari yake na kwamba wamekua wakifikisha ujumbe kwa
Wananchi juu ya mabadiliko hayo.
..........Bonyeza HAPA CHINI Umsikilize kwenye hii video ..
|
No comments:
Post a Comment