Beki wa
African Sports (kushoto) akimdhibiti Ibrahim Ajib wakati wa mchezo wa Simba vs
African Sports.
Bao la
ushindi la Simba SC, limekwamishwa wavuni na Haji Ugando na
kukamilisha kalamu ya mabao kwa siku ya leo.
Matumaini ya
Simba SC kuibuka kidedea kwa kutwaa ndoo ya ligi msimu huu yameibuka baada ya
mtani wao Yanga SC kukwama jijini Tanga mbele ya Coastal Union kwa kipigo cha bao
2-0.
Azam FC ambao leo,January 30,2016, wangecheza na Tanzania Prisons hawapo nchini hivyo mchezo
huo umeahirishwa hadi hapo watakaporejea nchini.
|
Haji Ugando
akijaribu kumtoka Ally Ahmed wa African Sports
Yanga SC bado
wanaongoza ligi wakiwa na pointi 39, Azam FC wako nafasi ya pili kwa pointi 39
sawa na Yanga SC lakini wao wanafaida ya mchezo mmoja mkononi ambao walitakiwa
wacheze leo.
|
Raia wa
kigeni waliovalia jezi nyekundu pia walikuwa wakishuhudia pambano kati ya Simba
SC dhidi ya African Sports.
Matokeo hayo
yanaiingiza Simba SC kwenye orodha ya timu ambazo zinawania ubingwa msimu huu
kutokana na tofauti ya pointi 3,Simba SC sasa wamefikisha pointi 36 lakini bado kuna mechi nyingi ambazo zinaweza
zikaamua nani ataibuka bingwa wa msimu huu.
|
Ibrahim Ajib
akichuana na Juma Shemvuni
Kocha Jackson
Mayanja ambaye anashikilia nafasi ya kocha mkuu kwa muda tangu kutimuliwa kwa
Dylan Kerr ameendelea kufurahia ushindi ndani ya klabu hiyo kwani ameshinda
mechi zote ambazo ameingoza Simba SC.
|
Mayanja
ameingoza Simba SC kwenye mechi tatu za ligi (Simba vs Mtibwa Sugar, Simba vs JKT
Ruvu na Simba vs African Sports) na kuvuna ponti 9 katika michezo hiyo
lakini paia alikiongoza kikosi hicho kwenye ushindi wa magoli 3-0 kwenye kombe
la FA dhidi ya Burkina Faso ya mkoani Morogoro.
|
MATOKEO NA
RATIBA LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA BARA 2015/2016.
Januari 30,
2016.
Coastal
Union 2-0 Yanga SC
Simba SC 4-0
African Sports
JKT Ruvu 0-0
Majimaji
Mwadui FC
1-0 Toto Africans
Kagera Sugar
Vs Mbeya City
Kesho;
Januari 31, 2016.
Mgambo JKT
Vs Ndanda FC
Mtibwa Sugar
Vs Stand United
|
No comments:
Post a Comment