USAFI DAY / UHURU DECEMBER 09:-Wafanyakazi wa Radio Free Africa Wafanya Usafi katika soko kuu la Kimataifa la Samaki Mwaloni jijini Mwanza. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, December 10, 2015

USAFI DAY / UHURU DECEMBER 09:-Wafanyakazi wa Radio Free Africa Wafanya Usafi katika soko kuu la Kimataifa la Samaki Mwaloni jijini Mwanza.

Pichani ni team ya Wafanyakazi wa Radio Free Africa/Mwanza kwa pamoja imesherekea sherehe za Uhuru wa Tanganyika, Disemba 09 kwa kufanya usafi katika katika soko kuu la Kimataifa la Samaki -Mwaloni jijini Mwanza, kama jinsi alivyoagiza Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuagiza kuwa siku ya Uhuru itumike kufanya usafi kutokana na kushamiri kwa uchafu katika mazingira yanayotuzunguka.

‘’-Tumeshiriki kusafisha maeneo mbalimbali ya soko hilo pamoja na eneo la fukwe za ziwa Victoria zilizopo karibu na soko hilo linalojumuisha wafanyabiashara wengi wa dagaa na samaki’’-Amesema Yusuph Magasha Meneja Msaidizi wa kituo, Radio Free Africa/Mwanza.

#Hapa Kazi tuu‘’Yusuph Magasha Meneja Msaidizi wa kituo, Radio Free Africa akiendelea na zoezi la Usafi katika soko la Mwaloni -Mwanza.

Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp .

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad