UCHAGUZI MKUU 2015 TANZANIA:-UKAWA na Wagombea wake hawa wa majimbo ya ubunge, matatu bado Utata. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, September 01, 2015

UCHAGUZI MKUU 2015 TANZANIA:-UKAWA na Wagombea wake hawa wa majimbo ya ubunge, matatu bado Utata.

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Profesa Abdallah Safari ambapo Maamuzi ya kupitisha wagombea hao yamesainiwa na Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Profesa Abdallah Safari, Katibu Mkuu wa chama cha National League for Democracy (NLD), Tozzy Matwanga na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Twaha Taslima.

 VYAMA vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) vimetangaza majina ya wagombea ubunge katika majimbo 262 huku majimbo matatu ya Mtwara Mjini, Serengeti na Mwanga yakisubiri muafaka.

Majimbo matatu yaliyobaki katika majadiliano baada ya kujitokeza wagombea wawili kwa kila jimbo huku kila mgombea akidai anakubalika kuliko mwenzake, ingawa vyama hivyo vilishayagawa majimbo hayo kwa chama kitakachogombea.

Jimbo la Serengeti wamejitokeza Marwa Ryoba (Chadema) na Mosena Nyambabe (NCCR-Mageuzi), jimbo la Mwanga wamejitokeza Henry Kilewo (Chadema) na Youngsaviour Msuya (NCCR-Mageuzi) na Mtwara Mjini wamejitokeza Maftaha Nachuma (CUF) na Hassani Uledi (NCCR-Mageuzi).

Wakati huohuo, majimbo ya Segerea na Kigamboni ya jijini Dar es Salaam tayari yamefanyiwa maamuzi kwa Julius Mtatiro (CUF) kubaki ndiye mgombea Segerea na Lucy Magereli wa Chadema kuwa mgombea jimbo la Kigamboni.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Dar es Salaam, wakati akitangaza majina hayo Katibu wa NCCR-Mageuzi, Dk. George Kahangwa amesema baada ya maamuzi hayo, haitarajiwi kutokea matatizo ya mivutano kwa viongozi wa ngazi ya mikoa hadi matawi wa vyama vya UKAWA.

Hatutarajii kuona viongozi wetu wa ngazi zote hasa zile za mikoa, wilaya, kata na matawi wanakuwa kikwazo cha kuyafikia malengo ya kuwakilishwa na mgombea mmoja,” amesema.

“Mgombea yeyote ambaye chama chake hakijaachiwa jimbo analogombea anatakiwa kujitoa katika nafasi yake hiyo na kumwachia mgombea wa chama kilichoachiwa jimbo hilo na kumpatia ushirikiano katika kampeni na utaratibu wa uchaguzi ili tushinde,” amesema Dk. Kahangwa.

Aidha, amesema viongozi kutoka vyama hivyo katika ngazi zote wanapaswa kuzingatia mwongozo wa awali uliosainiwa na Makatibu Wakuu wa vyama hivyo kuhusu kusimamisha wagombea katika nafasi ya udiwani.

Wakati muongozo huo ulipotolewa, viongozi hao walisema kwamba pale patakapokuwa na mvutano hata baada ya maamuzi ya jimbo limeachiwa chama gani kufanywa, basi viongozi wa kitaifa watakapokuwa kwenye kampeni, watazingatia maamuzi hayo na kuwatakia kura waliopitishwa kulingana na maamuzi yale.

WAGOMBEA UBUNGE WA UKAWA KATIKA KILA JIMBO LA TANZANIA BARA.

MARA        
                     
1.     Rorya             CDM STEVEN J OWAWA
2.     Tarime Mjini CDM ESTHER N MATIKO
3.     Tarime Vijijini CDM JOHN HECHE
4.     Serengeti CDM/NCCR MARWA RYOBA/MOSENA J.NYAMBABE
5.     Musoma Vijijini CDM ZAKARIA MBULA CHIRAGWILE
6.     Butiama           CDM YUSUPH R KAZI
7.     Bunda Mjini   CDM ESTHER BULAYA
8.     Mwibara         CDM HARUN D. CHIRIKO
9.     Musoma Mjini CDM VINCENT J NYERERE
10.                        Bunda Vijijini CDM SULEIMAN DAUDI

SIMIYU      
                     
1.     Bariadi             CDM GODWIN SIMBA
2.     Maswa magharibi CDM ABDALA PATEL
3.     Maswa mashariki CDM SYLVESTER KASULUMBAYI
4.     Kisesa             CDM MASANJA MANANI
5.     Meatu             CDM MESHACK OPULUKWA
6.     Itilima             CDM MARTINE MAGILE
7.     Busega           CUF JUMA A MAGOMA

SHINYANGA   
                       
1.     Solwa             CDM JAMES MSHANDETE
2.     Msalala           CDM PAUL MALAIKA
3. Kahama Mjini  CDM         LEMBELI JAMES
3.     Kahama Vijijini CDM SIMON BUKAKIYE ISAYA
4.     Shinyanga Mjini CDM PATROAS PASCHAL K
5.     Kishapu         CDM FRED MPENDAZOE

MWANZA   
                             
1.     Ukerewe         CDM JOSEPH MKUNDI
2.     Magu             CDM KALWINZI NGONGOSEKE
3.     Nyamagana       CDM EZEKIA D. WENJE
4.     Kwimba           CUF JULIUS S OTTO
5.     Sumve           CUF RICHARD M NTUNDURU
6.     Buchosa         CDM MARTINE KASWAHILI
7.     Sengerema       CDM FRANSISCO SHEYJAMABU
8.     Ilemela           CDM HIGHNESS KIWIA
9.     Misungwi         CDM LEONIDAS KONDELA

GEITA    
                         
1.     Bukombe       CDM PROF. KULIKOYELA KAHIGI
2.     Busanda         CDM ALPHONCE C MAWAZO
3.     Geita Vijijini CUF SEVERINE M MAGESE
4.     Nyang’wale     CDM RICHARD MABULA
5.     Chato             CDM DR. BENEDICT LUKANIMA
6.     Mbogwe         CDM NICHOLAUS H MAGANGA
7.     Geita Mjini       CDM RODGERS LUHEGA

KAGERA     
                   
1.     Karagwe         CDM PRINCE RWAZO
2.     Kyerwa           CDM BATRINIHO LADISLAUS
3.     Bukoba Mjini CDM WILFRED LWAKATARE
4.     Bukoba Vijijini CUF BUBELWA KAIZA
5.     Nkenge         NCCR ANGELINA MUTAHIWA
6.     Muleba Kaskazini CDM ANSBERT NGURUMO
7.     Muleba Kusini CDM ALISTIDES KASHASILA
8.     Biharamulo       CDM DR. ANTHONY MBASSA
9.     Ngara             NCCR HELENA ADRIAN GHOZI

MBEYA  
                         
1.     Lupa               CDM NJELU KASAKA
2.     Songwe           CDM MPOKI MWANKUSYE
3.     Mbeya Mjini CDM JOSEPH MBILINYI
4.     Kyela               CDM ABRAHAM MWANYAMAKI
5.     Rungwe           CDM JOHN D MWAMBIGIJA
6.     Busekelo         CDM BONIPHACE A MWAMUKUSI
7.     Ileje               NCCR EMMANUEL MBUBA
8.     Mbozi Mashariki CDM PASCHAL HAONGA
9.     Momba           CDM DAVID E SILINDE
10.  Mbarali            CUF GAMDUST HAJI
11.  Mbeya Vijijini      CDM ADAM NZELA
12.  Tunduma       CDM FRANK MWAKAJOKA
13.     Vwawa         CDM FANUEL MKISI

IRINGA  
                        
1.     Ismani             CDM PATRICK OLE SOSOPI
2.     Kalenga           CDM MUSSA L MDEDE
3.     Mufindi kaskazini CDM JUMANNE K MASONDA
4.     Mufindi Kusini CDM FRANK MALATA
5.     Iringa Mjini       CDM PETER MSIGWA
6.     Kilolo             CDM BRIAN KIKOTI
7.     Mafinga Mjini CDM WILLE MUNGAI

NJOMBE   
                     
1.     Njombe Kusini CDM EMMANUEL MASONGA
2.     Lupembe       CDM EDWIN E SWALE
3.     Wanging’ombe CDM DISMAS A LUHWAGO
4.     Makete           CDM JACKSON T MOGELA
5.     Ludewa                   CDM ATHROMEO MKINGA
6.     Makambako     CDM MHEMA

RUKWA  
                        
1.     Nkasi Kusini CDM ALFRED DANIEL SOTOKA
2.     Kwela             CDM DANIEL NAFTAL NGOGO
3.     Nkasi Kaskazini CDM KESSY SOUD
4.     Sumbawanga Mjini CDM SADRICK MALILA
5.     Kalambo         CDM VICTOR MATENI

TANGA   
                        
1.     Handeni Mjini CUF REMMY A SHUNDI
2.     Handeni Vijijini CUF ROBINSON R KILANGO
3.     Kilindi             CDM JERADI K MREMA
4.     Pangani           CUF AMINA M MWIDAU
5.     Tanga Mjini   CUF MUSSA B MBAROUK
6.     Muheza           CDM ERNEST MSINGWA
7.     Bumbuli         CDM DAVID CHENYEGOHA
8.     Mlalo               CUF GOGOLO SECHONGE
9.     Lushoto         CUF ADAM KAONEKA
10.                        Korogwe Mjini NCCR ROSE MICHAEL LUGENDO
11.                        Korogwe Vijijini CDM EMMANUEL KIMEA
12.                        Mkinga         CUF BAKARI K MBEGA

KILIMANJARO 
                             
1.     Rombo           CDM JOSEPH SELASIN
2.     Mwanga CDM/NCCR HENRY KILEWO/ YOUNGSAVIOUR MSUYA
3.     Same Magharibi CDM CHRISTOPHER S MBAJO
4.     Same mashariki CDM NAGENJWA KABOYOKA
5.     Vunjo             NCCR JAMES F. MBATIA
6.     Moshi Vijijini CDM ANTHONY C KOMU
7.     Moshi Mjini   CDM JAFARY P MICHAEL
8.     Hai                 CDM FREEMAN A MBOWE
9.     Siha               CDM DR. GODWIN MOLLEL

ARUSHA  
                       
1.     Arumeru Mashariki CDM JOSHUA NASSARI
2.     Arumeru Magharibi CDM GIBSON MESIYEKI
3.     Arusha Mjini   CDM GODBLESS LEMA
4.     Longido         CDM OLE NANGOLE
5.     Monduli CDM         JULIUS KALANGA
6.     Karatu             CDM WILLE QAMBALO
7.     Ngorongoro       CDM ELIAS NGORISA

MANYARA 
                            
1.     Simanjiro       CDM JAMES OLE MILLYA
2.     Mbulu Vijijini CDM MIKEL PETRO AWEDA
3.     Hanang           CDM MAGOMA RASHID DERICK
4.     Babati Mjini     CDM PAULINE P GEKUL
5.     Babati Vijijini CDM LAURENT TARRA
6.     Kiteto             CDM KIDAWA ATHUMANI IYAVU
7.     Mbulu Mjini   CDM PAULO HERMAN SULLE

DAR ES SALAAM     
                      
1.     Ubungo           CDM SAED KUBENEA
2.     Kawe             CDM HALIMA JAMES MDEE
3.     Kinondoni       CUF MAULID SAID
4.     Segerea           CUF JULIUS MTATIRO
5.     Ukonga             CDM MWITA WAITARA
6.     Ilala               CDM MUSLIM HASSANALI
7.     Temeke           CUF ABDALLA MTOLEA
8.     Kigamboni       CDM LUCY MAGERELI
9.     Kibamba         CDM JOHN JOHN MNYIKA
10.                        Mbagala         CUF KONDO J BUNGO

PWANI  
                          
1.     Bagamoyo         CUF DR. ANDREA KASAMBALA
2.     Chalinze         CDM MATHAYO TM. TORONGEY
3.     Kibaha Mjini CDM MICHAEL PAUL MTALY
4.     Kibaha Vijijini CDM KINABO EDWARD KINABO
5.     Kisarawe       CUF RASHID M MZANGE
6.     Mkuranga         CUF ALLY UBUGUYU
7.     Rufiji Utete     CUF KULUTHUMU MCHUCHULI
8.     Mafia             CUF OMARY A KIMBAU
9.     Rufiji Kibiti       CUF ABDALLAH M ISMAIL

MOROGORO  
                       
1.     Gairo             CDM SALIM YUSUPH MPANDA
2.     Kilosa               CUF ABEID H MLAPAKOLO
3.     Mikumi             CDM JOSEPH HAULE
4.     Morogoro Kusini CDM DAVID LUKAGINGIRA
5.     Morogoro Mashariki CUF SALAMA O AWADH
6.     Kilombero         CDM PETER KIBATALA
7.     Mlimba           CDM SUZAN L. KIWANGA
8.     Mvomero         CDM OSWALD MLAY
9.     Ulanga Magharibi CDM ALPHONCE MBASSA
10.                        Ulanga Mashariki CDM PANCRAS KONGOLI
11.                        Morogoro Mjini CDM MARCOSSY ALBANIE

DODOMA 
                              
1.     Kondoa Mjini CUF YASIN S BAKARI
2.     Kondoa Vijijini CUF ALLY B KAMBI
3.     Chemba         CUF ROGATH A MHINDI
4.     Kibakwe         CDM MSAFIRI MZINGA
5.     Mpwapwa       CDM BARAKA
6.     Kongwa           CDM ESAU NGOMBEI
7.     Dodoma Mjini CDM SINGO BENSON KIGAILA
8.     Bahi               CDM MATHIAS LYAMUNDA
9.     Chilonwa         CDM JOHN CHOGONGO
10.                        Mtera           CDM CHRISTOPHER NYAMWANJI

SINGIDA 
                       
1.     Iramba magharibi CDM JESCA KISHOA
2.     Iramba mashariki CDM OSCAR KAPALALE
3.     Singida kaskazini CDM DAVID DJUMBE
4.     Singida Mashariki CDM TUNDU A LISSU
5.     Singida Magharibi CDM MARCO ALLUTE
6.     Manyoni magharibi CDM LUPAA DONALD
7.     Manyoni Mashariki CDM ALLUTE EMMANUEL
8.     Singida Mjini CDM MGANA MSINDAI

TABORA     
                   
1.     Bukene           CUF DR. GODBLESS MAGULA
2.     Nzega Mjini   CDM CHARLES MABULA
3.     Nzega Vijijini CUF KHAMIS IDD KATUGA
4.     Igunga           CDM NG’WIGULU KUBE
5.     Igalula             CUF MOHAMED S A MERJIBI
6.     Tabora Kaskazini CUF REHEMA H BUSHIRI
7.     Urambo           CDM SAMWELI NTAKAMLENGA
8.     Kaliua             CUF MAGDALEN SAKAYA
9.     Ulyankulu       CDM DEUS NGERERE
10.                        Sikonge         CDM HIJJA RAMADHANI
11.                        Tabora Mjini CUF PETER S. MKUFYA
12.                        Manonga       CDM ALLY KHALFANI NGUZO

KATAVI    
                      
1.     Mpanda Mjini CDM JONAS KALINDE
2.     Mpanda Vijijini CDM MUSSA MASANJA
3.     Katavi             CDM GEORGE SAMBWE
4.     Nsimbo         CDM GERALD KITABU
5.     Kavuu             CDM LAURENT SENGA

KIGOMA  
                      
1.     Buyungu         NCCR MATHUSELA A MAWAZO
2.     Mhambwe       NCCR FELIX F MKOSAMALI
3.     Kasulu Mjini NCCR GIDEON B BONIPHACE
4.     Kasulu Vijijini NCCR AGRIPINA Z BUYOGERA
5.     Kigoma Kaskazini CDM DR. YARED FUBUSA
6.     Kigoma Kusini NCCR DAVID Z KAFULILA
7.     Kigoma Mjini CDM         DANIEL LUMENYELA
8.     Manyovu       NCCR MUHANDISI MWOMELA

RUVUMA       
                         
1.     Tunduru Kaskazini CUF MANJORO D KAMBILI
2.     Peramiho       CDM ELASMO MWINGIRA
3.     Mbinga Magharibi CDM CUTHBERT S. NGWATA
4.     Mbinga Mashariki CDM EDWIN B. AKITANDA
5.     Namtumbo       CUF BONIFASIA A MAPUNDA
6.     Songea Mjini CDM JOSEPH FUIME
7.     Tunduru Kusini CUF SADICK B SONGONI
8.     Madaba           CDM EDSON MBOGORO
9.     Mbinga Mjini NCCR MARIO MILLINGA

MTWARA

1.     Newala Mjini CUF JUMA S MANGUYA
2.     Newala Vijijini CUF JAFAR S MNEKE
3.     Tandahimba   CUF KATANI A KATANI
4.     Mtwara Vijijini CUF RASHID NANDONDE
5.     Nanyamba       CUF HAKUNA MGOMBEA
6.     Mtwara Mjini CUF/NCCR MAFTAHA NACHUMA/HASSANI A ULEDI
7.     Nanyumbu     CUF MAJARIBU H LUPETO
8.     Lulindi             NLD MODESTA PONELA
9.     Masasi           NLD EMMANUEL MAKAIDI
10.                        Ndanda         NLD ANGELOUS THOMAS

LINDI    
                          
1.     Mtama                 CUF ISIHAKA R MCHINJITA
2.     Kilwa Kaskazini CUF VEDASTO E NGOMBALE
3.     Kilwa Kusini   CUF SELEMANI S BUNGALA
4.     Lindi Mjini     CUF SALUM BARWANY
5.     Ruangwa       CUF OMARY I MAKOTA
6.     Nachingwea   CUF JORDAI MEMBE
7.     Liwale             CUF ZUBERI M KUCHAUKA
8.     Mchinga         CUF HAMIDU H BOBALI


 PAPO KWA PAPO Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad