Baadhi ya
wanachama wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) wakiwa katika mkutano na mgombea
mwenza wa nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu jana
August 31,2015 katika Ukumbi wa NEC ofisi za makao Makuu ya CCM Dodoma.
|
Mgombea
mwenza wa nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu
akizungumza na akinamama wanachama wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) na kuwaomba
kushirikiana na kuhakikisha wanashinda na kupata heshima hiyo.
|
Mgombea
mwenza wa nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu
akizungumza na akinamama wanachama wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) na
kuwaomba kushirikiana na kuhakikisha wanashinda na kupata heshima hiyo.
|
Mgombea
mwenza wa nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu
akizungumza na akinamama wanachama wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) na
kuwaomba kushirikiana na kuhakikisha wanashinda na kupata heshima hiyo.
|
Baadhi ya
wanachama wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) wakiwa katika mkutano na mgombea
mwenza wa nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu jana
August 31,2015 katika Ukumbi wa NEC ofisi za makao Makuu ya CCM Dodoma.
Na Joachim
Mushi, Dodoma
MGOMBEA
mwenza wa nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu
amefanya mazungumzo na wanachama wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) na kuwaomba
kuitumia vema heshima na nafasi waliopewa akinamama nchini ya kushika nafasi ya
makamu wa rais kwa mara ya kwanza, hivyo kuhakikisha wanahamasisha wenzao ili
CCM iweze kushinda na wanawake kutwaa heshima hiyo.
Bi. Suluhu
amesema hayo alipokuwa akizungumza na akinamama wa UWT mkoani Dodoma ikiwa
pamoja na kutaja kipaumbele ambapo kimewekwa kwa akinamama katika ilani mpya ya
CCM katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 25, 2015.
Alisema atatumia nafasi
yake kushawishi akinamama kipata vifaa na mazingira rafiki ya kuendesha kilimo
cha kisasa ili waweze kukuza uchumi wao, pia kuwawezesha katika vikundi vya
ujasiliamali ikiwa ni pamoja na kukomesha usumbufu ambao akinamama
wafanyabiashara wamekuwa wakibughuziwa na mgambo wa jiji.
Mgombea huyo
alisema kupitia vikundi akinamama watawezeshwa na fungu la fedha shilingi
milioni hamsini fedha ambazo zitatolewa kila kijiji maalumu kwa ajili ya
kuwawezesha akinamama pamoja na vijana ili waweze kukuza mitaji yao.
Pamoja na
hayo Bi. Suluhu alisema Serikali watakayoiunda itashughulikiwa changamoto anuai
wanazokumbana nazo walemavu hasa akinamama ili kuwawezesha na wao katika
ushindani. “…Kwa upande wa kilimo nitahakikisha nachochea kidogo kidogo ili
wanawake wapate vitu kama pembejeo na vifaa vingine kuwawezesha kuendesha
kilimo cha kisasa,” alisema.
|
Mmoja wa
wajumbe wa kamati ya taifa ya kampeni za CCM, Bi. Ummy Mwalimu akitoa neno
katika mkutano na wanachama wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) kwenye Ukumbi wa
NEC ofisi za makao Makuu ya CCM Dodoma.
|
Baadhi ya
wajumbe wa kamati ya taifa ya kampeni za CCM (mbele) walioambatana na mgombea
mwenza, Bi. Samia Suluhu wakiwa katika mkutano na wanachama wa Umoja wa
Wanawake wa CCM (UWT) katika Ukumbi wa NEC ofisi za makao Makuu ya CCM Dodoma.
|
Mke wa
waziri Mkuu wa Tanzania, Mama Tunu Pinda akizungumza na wanachama wa Umoja wa
Wanawake wa CCM (UWT) kabla ya mkutano huo na mgombea mwenza wa nafasi ya urais
wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu jana August 31,2015 kuanza katika Ukumbi wa NEC
ofisi za makao Makuu ya CCM Dodoma.
|
Mmoja wa
wajumbe wa kamati ya taifa ya kampeni za CCM, Bi. Asumpta Mshana akitoa neno
katika mkutano na wanachama wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) kwenye Ukumbi wa
NEC ofisi za makao Makuu ya CCM Dodoma.
|
Mwenyekiti
wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) mkoani Dodoma, Bi. Salome Kiwaya akizungumza
kabla ya mkutano huo na mgombea mwenza wa nafasi ya urais wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu jana August 31,2015 kuanza katika Ukumbi wa NEC ofisi za makao
Makuu ya CCM Dodoma.
|
Baadhi ya
wanachama wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) wakiwa katika mkutano na mgombea
mwenza wa nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu jana
katika Ukumbi wa NEC ofisi za makao Makuu ya CCM Dodoma.
|
Baadhi ya
wawakilishi wa makundi anuai katika wanachama wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT)
wakitoa neno kuwawakilisha wajumbe wenzao katika mkutano huo na mgombea mwenza
wa nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu jana August 31,2015 katika
Ukumbi wa NEC ofisi za makao Makuu ya CCM Dodoma.
|
Makundi
ambalimbali ya akinamama wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) mkoani Dodoma,
wakimpa zawadi mgombea mwenza wa CCM nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu katika
Ukumbi wa NEC ofisi za makao Makuu ya CCM Dodoma.
Alisema
ilani ya CCM imetoa kipaumbele kwa huduma za afya hasa huduma za mama na mtoto
ikiwa ni kutambua changamoto na matatizo wanayokumbana nayo akinamama eneo
hilo. Alisema atadhibiti rushwa na matumizi mabaya ya dawa zinazopelekwa wizara
ya afya kuhakikisha zinafanya kazi kama ilivyokusudiwa na kudhibiti urasimu.
Aliongeza
kuwa baada ya ujenzi wa shule za kata kufanikiwa akiingia madarakani anaongeza
nguvu katika ujenzi wa mabweni ya wasichana ili kukabiliana na changamoto ya
mimba kwa wanafunzi wasichana ambazo zimekuwa zikichangiwa na wao kutembea
umbali mrefu na kupata changamoto njiani.
Aidha
aliongeza kuwa ili kuonesha Serikali ya CCM inawajali walimu itaunda chombo
maalumu ambacho kitakuwa na kazi ya kushughulikia matatizo ya walimu pamoja na
kukiwezesha kuhakikisha kinatimiza majukumu yake kiufasaha.
Aliwaomba
akinamama kushirikiana kufanya kampeni na kuhakikisha CCM inashinda hivyo
akinamama kupata fursa hiyo waliyopewa na CCM kwa sasa.
“…Naombeni tushirikiane
wote kufanya kampeni nyumba kwa nyumba, kitanda kwa kitanda na shuka kwa shuka
ili kuhakikisha tunashinda maana hii ni zawadi kwa akinamama tujitahidi tuweze
kushinda nafasi hii,” alisema Bi. Suluhu.
|
Baadhi ya
wanachama wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) wakiwa katika mkutano na mgombea
mwenza wa nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu jana
katika Ukumbi wa NEC ofisi za makao Makuu ya CCM Dodoma.
|
Baadhi ya
wawakilishi wa makundi anuai katika wanachama wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT)
wakitoa neno kuwawakilisha wajumbe wenzao katika mkutano huo na mgombea mwenza
wa nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu jana katika
Ukumbi wa NEC ofisi za makao Makuu ya CCM Dodoma.
|
Baadhi ya
wanachama wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) wakiwa katika mkutano na mgombea
mwenza wa nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu jana
August 31,2015 katika Ukumbi wa NEC ofisi za makao Makuu ya CCM Dodoma.
*Imeandaliwa
na www.thehabari.com
|
No comments:
Post a Comment