ALIYEKUWA
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk Willibrod Slaa
ametangaza rasmi kuachana na siasa.
Amesema
hatua hiyo inatokana na hatua ya CHADEMA kumkaribisha Edward Lowassa bila
masharti na baadaye kumteua kuwa mgombea urais wa chama hicho.
Lowassa
ambaye ni mgombea urais wa CHADEMA, anaungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja
wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) ambavyo ni CHADEMA yenyewe, CUF, NCCR-Mageuzi
pamoja na NLD.
Katika
mkutano wake na waandishi wa habari jana September 01,2015 ,jijini Dar es
Salaam, Dk. Slaa amesema hatojiunga na chama chochote cha siasa na badala yake
ataendelea kuwatumikia wananchi nje ya siasa.
Hata hivyo
amesema uamuzi huo unatokana na kutoridhishwa na hatua zilizochukuliwa na
viongozi wakuu wa CHADEMA akiwemo mwenyekiti wake, Freeman Mbowe kupokea
wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliowahi kutuhumiwa na chama hicho.
BOFYA HAPA CHINI KUTAZAMA VIDEO YA MKUTANO WAKE NA WAANDISHI WA HABARI.
|
No comments:
Post a Comment