KAMPENI CCM 2015:-CCM Kuja na Muarobaini Mapigano ya Wafugaji na Wakulima. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, September 02, 2015

KAMPENI CCM 2015:-CCM Kuja na Muarobaini Mapigano ya Wafugaji na Wakulima.

Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu akiwa amepokea kadi kutoka kwa wanachama wa CHADEMA waliojiunga na CCM baada ya kukihama chama hicho.

Baadhi ya wanaCCM na wananchi wakiwa katika mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu.

Mgombea Mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu amesema Serikali itakayoundwa na chama hicho endapo itashika dola katika Uchaguzi Okuu wa Oktoba, 2015 itahakikisha inapima ardhi yote ya vijiji pamoja na kuainisha mipaka ili kukomesha migogoro ya ardhi.

Bi. Suluhu ametoa kauli hiyo alipokuwa akinadi ilaya ya CCM katika Majimbo mawili tofauti ya Kongwa na Chilonwa Mkoa wa Dodoma ikiwa ni mwendelezo wa ziara zake za kufanya kampeni kuwashawishi Watanzania waweze kuipa ridhaa tena Chama Cha Mapinduzi ili kiunde Serikali na kuwatyumikia wananchi.

Mgombea huyo mwenza wa urais akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Chilonwa Kijiji cha Nzali alisema Serikali ya CCM kwa kushirikiana na halmashauri itaipima ardha ya vijiji na kuweka mipata hasa maeneo sugu ya migogoro kama Kongwa na Kiteto ili kuzuia migogoro na mapigano kwa jamii hizo mbili.

Alisema mara baada ya kupima ardhi na kuweka mipaka kati ya maeneo ya wakulima na wafugaji watahakikisha mipaka hiyo inatambulika na kuheshimiwa na jamii zote mbili ili kuzuia migogoro na mapigano ambayo yamekuwa na uhasama mkubwa na kupoteza uhai na mali za raia wasio kuwa na hatia katika maeneo yenye mgogoro...BOFYA HAPA USOME ZAIDI TAARIFA HII.


Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad