Mamlaka ya
Mawasiliano Tanzania (TCRA) inapenda kutoa taarifa kuwa kuanzia leo tarehe
10 Septemba 2015, na katika kipindi chote cha kampeni za uchaguzi mkuu 2015, watu ambao sio wagombea wa udiwani,
ubunge,urais, wasemaji rasmi wa vyama au watu wasioteuliwa na vyama vya siasa
kama wawakilishi hawataruhusiwa kushiriki katika vipindi vya moja kwa moja
(Live Programmes) vinavyohusu shughuli za uchaguzi vitakavyorushwa
na vituo vya utangazaji.
Utaratibu
huu unazingatia Kanuni Za Huduma Za Utangazaji (Maudhui),Utangazaji Wa Uchaguzi Wa Vyama Vya Siasa), 2015, Kanuni ya 4 (f),
(h),(i), 5(b), (d), (e) and (f).
Hatua hii
inachukuliwa na Mamlaka ili kuweka utaratibu mzuri wa kufanya kampeni za
uchaguzi ziwe za amani na utulivu.
Hatua kali
za kisheria zitachukuliwa dhidi ya kituo cha utangazaji kitakacho kwenda
kinyume na utaratibu huu..
IMETOLEWA NA:
Mkurugenzi Mkuu
MAMLAKA YA
MAWASILIANO TANZANIA
Tarehe,
11/09/2015
Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
No comments:
Post a Comment