Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akimnadi kwa
wananchi, Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigoma Kusini katika mwamvuli wa Ukawa
kupitia Chama cha NCCR-Mageuzi, David Kafulila, katika Mkutano wa hadhara wa
Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Nguruka Kati, jana Septemba 4, 2015.Picha
na Othman Michuzi, Kigoma.
Katika
mkutano huo wa Kampeni za UKAWA 2015,Mgombea wa urais ,Bw. Edward Lowassa
amebainisha vipaumbele vyake iwapo wananchi watampigia kura ya NDIYO kwa
kuhakikisha elimu ya awali hadi chuo kikuu inatolewa bure bila kuwepo kwa
michango kwa mwananchi.
Pia amesema
katika utawala wake atahakikisha kuwa wakulima wanaondolewa ushuru pamoja na
vikwazo vya kuuza mazao nje ya nchi sambamba na kuhakikisha anaongeza ajira kwa
vijana mkoani humo kwa kuweka viwanda vya kusindika mafuta ya mawese,sambamba
na serikali yake itatunga sera kuhakikisha nyumba za nyasi zinaondolewa nchi
nzima na wananchi wanakuwa na makazi bora.
|
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akikaribishwa na
Mwenyeji wake, Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigoma Kusini katika mwamvuli wa
Ukawa kupitia Chama cha NCCR-Mageuzi, David Kafulila, mara baada ya kuwasili
kwenye Uwanja wa Nguruka Kati, kulikofanyika Mkutano wa Kampeni za Mgombea
huyo, jana Septemba 4, 2015.Katikati ni Mwenyekiti wa CHADEMA, Mh. Freeman
Mbowe. Picha na Othman Michuzi, Kigoma.
|
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akipokea saluti
kutoka kwa Askari Polisi, wakati alipowasili kwa Helkopta, kwenye Uwanja wa
Nguruka Kati, Jimbo la Kigoma Kusini, kulikofanyika Mkutano wa Kampeni za
Mgombea huyo, jana Septemba 4, 2015.Picha na Othman Michuzi, Kigoma.
|
No comments:
Post a Comment