KAMPENI UKAWA 2015:-Taswira ya Mkutano wa Mh. Edward Lowassa Mkoani Njombe August 31,2015 na na namna alivyojipanga kuwatumikia Wwatanzania. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, September 01, 2015

KAMPENI UKAWA 2015:-Taswira ya Mkutano wa Mh. Edward Lowassa Mkoani Njombe August 31,2015 na na namna alivyojipanga kuwatumikia Wwatanzania.


Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwahutubia wananchi waliofurika kwa wingi wakati wa mkutano wa kampeni kwenye Mji wa Makambako,  Mkoani Njombe jana Agosti 31, 2015. 

Katika hotuba yake, Mh. Lowassa amewatoa hofu wana CCM wanaotaka kujiunga na Ukawa kutoogopa kuchukua uamuzi huo kwani huu ni mwaka wa mabadiliko. 

Pia amewaomba Watanzania wanaomuunga mkono katika mikutano yake ya hadhara kutoishia hapo na badala yake kujitokeza kwa wingi katika Uchaguzi wa Mwaka huu wa Oktoba 25 mwaka huu.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akimnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Makambako, Mhema Oraph, wakati wa Mkutano wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Polisi Makambako, Mkoani Mkoani Njombe jana Agosti 31, 2015.

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwasili kwenye Uwanja wa Polisi Makambako, Mkoani Mkoani Njombe jana Agosti 31, 2015, kulikofanyika Mkutano wa Kampeni, na kuhudhuliwa na umati wa wananchi wakazi wa maeneo mbali mbali ya Mji wa Makambako.




Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akipongeza na baadhi ya Wagombea Udiwaki wa Kata mbali mbali za Mji wa Makambako, Mkoani Njombe baada ya kuhutubia Mkutano wake wa Kampeni.

Mgombea urais wa vyama vinavyounda UKAWA Mh Edward Lowassa ameendelea kunadi sera zilizoko kwenye ilani ya umoja wa vyama vyao katika wilaya za mkoa wa Njombe huku wananchi, viongozi, na wagombea wa UKAWA wakiwataka watanzania kutambua kuwa hatua ya wagombea wa CCM ya kuendelea kulalamika na kutoa ahadi ni kielelezo cha kutosha kuonyesha kuwa hawana  jipya na wamepoteza sifa za kuongoza. 

Pia  Mh.Lowassa alieleza sera zilizoko kwenye ilani ya UKAWA na namna alivyojipanga kuwatumikia watanzania kama wakimchagua kuwa rais likiwemo la kuondoa tabaka la maskini na tajiri sambamba na kuwahakikishia watanzania suala la amani.

Waliowahi kuwa mawaziri mkuu wa serikali ya CCM, Mh Fredrick Sumaye na Waziri wa mambo ya ndani ,Laurence Masha ambao wamehamia UKAWA wakaendelea kuweka wazi umuhimu wa watanzania kupokea mabadiliko.

Baadhi ya wananchi wamesema baada ya kusikia sera za UKAWA wana matumaini makubwa ya kuondokana na matatizo waliyonayo chini ya Mh Edward Lowassa ambaye wanajua utendaji wake.


Habari na :-ITV.
  

PAPO KWA PAPO Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad