Droo ya
makundi ya ligi hiyo, inatarajiwa kufanyika leo hii August 27,2015 ambapo Kila
Chungu kitakuwa na Jumla ya Timu 8 ambapo kila Chungu kitatoa Timu 1 kuunda
Kundi moja la Timu 4 lakini Klabu toka Nchi moja hazitawekwa katika Kundi moja.
Hivyo,
Mabingwa Watetezi FC Barcelona, Chelsea, Bayern München, Juventus, Benfica, Paris
Saint-Germain, Zenit and PSV Eindhoven zote zipo Chungu Namba 1 na hivyo
haziwezi kupambanishwa.
Pia safari
hii Bingwa wa EUROPA LEAGUE 2014/2015, ambae ni Sevilla, ameingizwa moja kwa
moja kwenye UEFA CHAMPIONS LEAGUE na hii imeifanya Spain iwe Nchi ya kwanza
kabisa kuwa na Timu 5 kwenye UEFA CHAMPIONS LEAGUE ukizijumuisha Barcelona,
Real Madrid, Atletico Madrid na Valencia iliyofuzu kutoka Mechi za Mchujo.
TIMU ZIPI ZIPO
KWENYE CHUNGU KIPI.
***Kila Chungu kina
Jumla ya Timu 8 mbapo kila Chungu kitatoa Timu 1 kuunda Kundi moja la Timu 4
isipokuwa Timu za Nchi moja hazitawekwa Kundi moja.
CHUNGU NAMBA 1: Barcelona,
Chelsea, Bayern München, Juventus, Benfica, Saint-Germain, Zenit St Petersburg,
PSV Eindhoven.
CHUNGU 2: Real Madrid,
Atlético Madrid, FC Porto, Arsenal, Valencia, Manchester City, Manchester
United, Bayer Leverkusen
CHUNGU 3: Olympique
Lyonnais, Dynamo Kyiv, Olympiacos, Galatasaray, Roma, Shakhtar Donetsk,
Sevilla, CSKA Moscow
CHUNGU 4: Borussia
Mönchengladbach, Wolfsburg, Dinamo Zagreb, Maccabi Tel-Aviv, Gent, Malmo,
Astana, BATE Borisov
TAREHE MUHIMU:
-Droo Hatua ya
Makundi: Agosti 27,2015.
-Ratiba Mechi za
Makundi:
Mechidei 1: 15/16
Septemba
Mechidei 2: 29/30
Septemba
Mechidei 3: 20/21
Oktoba
Mechidei 4: 3/4
Novemba
Mechidei 5: 24/25
Novemba
Mechidei 6: 8/9
Decemba
Raundi za Mtoano:
-Droo ya Raundi ya
Mtoano ya Timu 16: Desemba 14,2015
**Mechi Februari
16/17/23/24 na Marudiano Machi 8/9/15/16
-Droo ya Robo
Fainali: Machi 18,2016
**Mechi Aprili 5/6
na Marudiano Aprili 12/13
-Droo ya Nusu
Fainali: Aprili 15,2016
**Mechi Aprili 26/27
na Marudiano Mei 3/4
FAINALI
Mei 28,2016.
San Siro, Milan,
Italy
PAPO KWA PAPO Pata Picha, Habari za Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo
na Nyingine kwa kujiunga na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia
tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
No comments:
Post a Comment