![]() |
|
Sehemu ya
Viongozi wa CHADEMA waliokuwepo kwenye hafla hiyo.
|
![]() |
|
Baadhi ya
Wadau walioambatana na Mh. Lowassa….
BOFYA
HAPA KWA PICHA ZAIDI.
HATIMAYE
Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa leo Agosti 01,2015 amerejesha fomu ya
kuomba uteuzi kuomba urais kupitia tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA).
Aidha, katika urejeshaji wa fomu Lowassa
amepata udhamini kutoka mikoa 32 ambao amedhaminiwa na wanachama zaidi ya
milioni 1.6
Kwa mujibu
wa Mkurugenzi wa Organaizesheni na Uchaguzi, Benson Kigaila amesema, wadhamini
hao wamepatikana kutoka katika Kanda 10 na Mikoa 32 kwa nchi nzima.
“Sasa safari
ya matumaini kupitia CCM imeishia njiani,safari ya uhakika kupitia Chadema
imefika na kipindi hiki lazima kieleweke na tunaenda kuiondoa CCM madarakani
asubuhi kweupe”,amesema Kigaila.
Ameongeza
kuwa wanachama kutoka mikoa yote walikuwa wakitamani Lowassa apitie mikoa yote
ili kumdhamini kutokana na muda mchache wameamua kumdhamini kupitia njia ya
simu.
Kigaila
ambae pia ni Mkurugenzi wa Kanda wa Mambo ya Uchaguzi wa chama hicho amesema
wanachama wasijali chochote kwa kuwa baada ya mkutano mkuu kumpitisha mgombea
ambao unatarajia kufanyika Agosti nne atachanja mbuga kuzunguka mikoa yote.
Nae Profesa
Abdallah Safari ambae ni Makamu Mwenyekiti wa Chama Bara amesema amemshukuru
Lowassa kwa kurejesha fomu hiyo kwa kuwa baadhi ya watu walidhani angeingia
mitini kwa hiyo sasa tunajiandaa kwenda kuchukua dola.
Nae Naibu
Katibu Mkuu Zanzibar Salum Mwalimu amesema chama tawala hawawezi
kuwasambaratisha chadema na kuja kwa Lowassa ni mpango wa mungu na nyama zote
walizopanga hazitafanikiwa.
Pata
Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori
inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|











No comments:
Post a Comment