Mtendaji wa
Kata ya Lusahunga Bw Jeremiah Kasaizi amesema tukio hilo limetokea jana August 23,2015 majira
ya Saa 4 Usiku na kwamba magari hayo yalikuwa yamebeba Mafuta, Nafaka na Saruji.
Amesema moto
huo ulipungua baada ya Jeshi la Zimamoto kufika kutoka mjini Bukoba ambapo hata
hivyo halikuwa na vifaa vya kutosha na hivyo wananchi kusaidia kuuzima moto huo
kwa kutumia mchanga.
Mmoja wa
madereva wa magari hayo amesema hasara iliyopatikana kwenye gari lake ni zaidi
ya Sh Milioni 80 na kwamba moto huo umetokea wakati watu wakiuziana mafuta .
Kamanda wa
Polisi wa Mkoa wa Kagera Bw Augustino Olomi amethibitisha kutokea kwa tukio
hilo na kwamba hakuna mtu aliyefariki bali dereva mmoja amepelekwa kwenye zahanati
ya Nyakanazi baada ya Presha kupanda…Habari kwa hisani ya RADIO KWIZERA FM
|
Taswira pichani ya magari 7 ya mizigo na mafuta yaliyokuwa yameegeshwa
eneo la nyakanazi yakiwa yameteketea kwa moto,uliosababishwa wakati watu wakiuziana mafuta .
|
PAPO KWA PAPO Pata Picha, Habari za Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo
na Nyingine kwa kujiunga na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia
tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp
+255789925630. |
No comments:
Post a Comment